Friday, June 29, 2012

* Kampuni ya Simu ya tiGO yaendeleza Shangwe kwa Wateja wake Mjini Kahama





 
Picha mbalimbali zinazoonyesha matukio tofauti yaliyofanyika wakati wa tamasha la Tigo lililofanyika Mjini Kahama katika eneo la stendi ndogo, katika tamasha hilo burudani zilitolewa na kikundi cha sarakasi na msanii H. Baba kutoka mjini Dar es Salaam aliwapagawisha kwa Burudani safi ya Muziki wateja wa Kampuni hiyo.

Pia wateja wa Tigo walipata fursa ya kushinda zawadi mbalimbali kama vile simu, Tshirt na kofia za TigoVilevile huduma za Tigo zilipatikana katika viwanja hivyo.

* tiGO yamkabidhi hundi ya Shillingi milioni Mshindi wa Promosheni inayoendelea ya Tigo-Beatz Bi Zumra Mohammed


Tigo Public Relations Officer, Ms ALICE MARO (left) hands over a dummy cheque of Sh 10,000,000 to Ms ZUMRA MOHAMMED during a press conference held in Moshi.

Ms MOHAMMED was selected randomly during a live draw last week as the first winner of  the on-going Tigo Beatz promotion.

Standing in the centre is Mr ABUBAKARI MASSOLI, Tigo Customer Service and Sales Representative, Kilimanjaro. Far right is Mr MOHAMMED HASSAN RAJAB, Administrative, Kilimanjaro.


Ms ZUMRA MOHAMMED, the first winner of the on-going Tigo Beatz promotion, proudly holds up a dummy cheque of Sh 10,000,000 from Tigo.

Thursday, June 14, 2012

* Waziri wa Habari Azungumza na Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali Jijini Mwanza


Waziri wa Habari vijana, Utamaduni na Michezo Dakta FENELLA MUKANGARA akiongea na maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali jijini Mwanza.

Pamoja na mambo mengine amewataka maafisa hao kuielimisha jamii kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo yanayofanywa na serikali kupitia vyombo vya habari.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo SETH KAMUHANDA mstari wa kwanza) akifuatilia mada  kuhusu changamoto zinazoikabili Tanzania katika kuhama kutoka mfumo wa Analojia  kwenda Digitali kufikia mwaka 2012 katika Kikao kazi cha Maafisa habari na Mawasiliano wa Serikali ijini Mwanza.

Wengine wanaoonekana kwa nyuma ni maafisa habari na mawasiliano wa Serikali.


Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali wakifuatilia kwa makini hotuba iliyokuwa ikitolewa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ijini Mwanza.

Wednesday, June 13, 2012

* Mabondia Francis Cheka na Japhet Kaseba Kuzichapa Julai 7 mwaka huu


Mabondia FRANCIS CHEKA (kushoto) na JAPHET KASEBA wakitunishiana misuli wakati wa utambulisho wa mpambano wao unaotarajia kufanyika Julai 7 katika uwanja mpya wa taifa ambapo kutakuwa na burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii mbalimbali wakiongozwa na Diamond.

Pia kutakua na mechi ya Bongo Movie na wasanii wa Bongo Fleva watakapochuana kwa mara nyingine katika mpambano ulioandaliwa na Global na kuratibiwa na KAIKE SIRAJU utakuwa ni mpambano wa kwanza wa Masumbwi kufanyika katika uwanja mpya wa Taifa
Baadhi ya mabondia watakaosindikiza mpambano huo ni  Adiphoce Mchumia tumbo atakaedundana na Ramadhani Kido wakati Amos Mwamakula ataoneshana kazi na Rashini Ali huku Mkongo Kanda Kabongo akizipiga na  Said Mbelwa wakati bondia chipukizi kutoka kambi ya masumbwi ya Ilala inayonolewa na Kocha Mkongwe Habibu Kinyogoli Masta na Kocha maarufu Rajabu Mhamila 'Super D'  watampandisha bondia Ibrahimu Class kuoneshana kazi na Sadiki Momba.

Friday, June 8, 2012

* Rais Jakaya Kikwete awaapisha Majaji wawili na Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama



Rais Dkt JAKAYA KIKWETE akimwapisha SEMISTOCLES KAIJAGE (kulia) kuwa jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Kabla ya uteuzi huo KAIJAGE alikuwa jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam.

Jaji wa Mahakama ya Rufani MUSSA KIPENKA akisaini hati ya kiapo mara baada ya kuapishwa na Rais  Dkt JAKAYA KIKWETE Ikulu jijini Dar es Salaam, anayeshuhudia ni jaji mkuu wa Tanzania MOHAMMED CHANDE OTHMAN.

Rais JAKAYA KIKWETE akimwapisha EDWARD RUTAKANGWA kuwa kamishna  wa Tume ya Utumishi wa Mahakama katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dares Salaam.

* Rais Dakta Ali Shein kwa Nyakati tofauti akutana na Balozi wa Sweden, pia ameagana na Balozi wa Msumbiji aliyemaliza muda wake


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt ALI MOHAMMED SHEIN akisalimiana na Balozi wa Msumbiji Nchini Tanzania AMOUR ZAKARIA aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar kumuaga Rais, baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini.




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt ALI MOHAMMED SHEIN akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini Tanzania LENNARTH HJELMAKER aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar kujitambulisha kwa  Rais.

Thursday, June 7, 2012

* Kampuni ya Simu ya tiGO yatoa Zawadi na Burudani Mbalimbali kwa Wateja wake Wilayani Babati





Picha hizi zinaonyesha matukio mbalimbali yaliyofanyika wilayani Babati, ambapo kampuni ya tiGo iliwapatia wateja burudani kutoka kwa mwanamuziki H.Baba , Pia wateja walipata fursa ya kupata huduma mbalimbali kutoka kwenye vibanda vya tiGo vilivyopatikana viwanjani hapo, ambapo Zawadi kama T-shirt za tiGo, Simu na kofia zilitolewa katika tamasha hilo.