Friday, July 8, 2011

* Simba na Yanga Zatinga Fainali ya Michuano ya Kombe la Kagame,Kukipiga Jumapili katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam

  
 
Rais wa Rwanda PAUL KAGAME ndie Mdhamini wa Michuano ya Kombe la Kagame


Kikosi cha Timu ya SIMBA Sports Club  ambao ni maarufu kama Wekundu wa Msimbazi watakaokipiga na Mahasimu wao wakubwa YANGA Sports Club watoto wa Jangwani katika Fainali ya Kombe la Kagame.


Kikosi kamili YANGA Sports Club ambao ni maarufu kwa jina la watoto wa Wajangwani ambao watakabiliana na mahasimu wao wa Enzi SIMBA Sports Club katika Michuano ya Kombe la Kagame itakayopigwa siku ya Jumapili katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.

Wednesday, July 6, 2011

* Mtoto Felix Finkbeiner akiwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Tayari kuanza Ziara yake ya kupanda miti katika Shule za Msingi hapa nchini


Mtoto FELIX FINKBEINER kutoka Nchini Ujerumani  Kulia akiwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam akiwa tayari kuanza Ziara ya Upandaji wa Miti katika Shule za Msingi kupitia kampeni yake inayoitwa Plant the Planet Stop talking ambapo anatazamiwa kuelekea Visiwani Zanzibar na Baadae ataenda mkoani Arusha pia anatazamiwa kupanda Mlima Kilimanjaro akiwa katika ziara yake hapa nchini.

Tuesday, July 5, 2011

* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Gharib Bilal pamoja na Makamu wa Kwanza wa Rais wa ZANZIBAR Maalim Seif Shariff Hamad Wakutana katika Viwanja vya Saba saba.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akisalimiana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim SEIF SHARIFF HAMAD wakati walipokutana kwenye viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere katika Maonyesho ya 35 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

* Mashindano ya Pikipiki yafana Viwanja vya Tanganyika Packers kawe Jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki hii


Waendesha Pikipiki wakianza mwendo kwa pamoja wakati wakishindana katika mazoezi yao ya kujiweka fiti kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers Kawe jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita.


Waendesha Pikipiki wakianza mwendo kwa pamoja wakati wakishindana katika mazoezi yao ya kujiweka fiti kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers Kawe jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita.

Waendesha Pikipiki, Adil Othman (mbele) akichuana na Ludan Volvo, wakati wa mazoezi yao ya kujiweka fiti kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers Kawe jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. Adil ni mtaalam wa kutumia Pikipiki yenye matairi manne aina ya Quad Bike na Volvo ni mtaalam katika pikipiki ya matairi mawili, hapa wakionyeshana ujuzi.

                                    


Saturday, July 2, 2011

* Makamu wa Rais Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL azindua rasmi Maonesho ya 35 ya Biashara ya Kimataifa Jijini Dar es Salaam


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL, akizindua rasmi maonyesho ya 35 ya Biashara  ya Kimataifa , wakati alipotembeleea maonyesho hayo katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere Barabara ya Kilwa Dar es Salaam.

 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akimkabidhi Tuzo ya ushindi wa kundi la Engineering Products Mkurugenzi Mkuu wa Sido, MIKE LAISER,wakati wa ufunguzi rasmi wa maonyesho ya 35 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.


Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye pia ni Mkurugenzi wa Bendi ya Mjomba MRISHO MPOTO akitoa burudani mbele ya mgeni rasmi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL wakati wa uzinduzi wa maonyesho ya 35 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika Jijini Dar es Salaam.

* Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim SEIF SHARIFF HAMAD akutana na Wakurugenzi wa Bodi ya Kamisheni ya Utalii Zanzibar

 
Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim SEIF SHARIF HAMAD akipokea Kabrasha la mpango mkakati la maendeleo ya Utalii Zanzibar kutoka Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, ISSA AHMEID OTHMAN ofisini kwake Migombani.

* Shirika la Kimataifa la OXFAM lazindua Shindano la Mama Shujaa wa Chakula

Shirika la kimataifa la kukabiliana na umasikini wa Chakula la OXFAM limezindua Shindano la Mama Shujaa wa Chakula,ambalo litakuwa likifanyika kila mwaka kwa lengo la kuwatambua na kuwaenzi wanawake wazalishaji wa Chakula.

Shindano hilo litawahusisha akina mama ambao ni wafugaji na wakulima wadogo wa mazao ya Chakula kutoka katika mikoa na maeneo mbalimbali hapa nchini.

Shindano hilo limezinduliwa Jijini Dar es Salaam na Mcheza tamthilia maarufu ya Sex and the City kutoka Holywood nchini Marekani KRISTIN DAVIS huku akishirikiana na Balozi wa Kampeni ya Grow wa OXFAM ambae pia ni Mcheza Filamu wa Hapa nchini STEVEN KANUMBA.

Kwa mujibu wa OXFAM Shindano hilo litakuwa la wazi ambapo wananchi watakuwa wakishiriki kwa kuwapigia akina mama 10 watakaopita katika hatua ya awali mara baada ya kukamilisha utaratibu wa kujaza Fomu za ushiriki wa Shindano hilo.


Kutoka kulia ni Mcheza filamu wa Tanzania STEVEN KANUMBA kati kati ni Mcheza tamthilia maarufu kutoka Holywood Marekani KRISTIN DAVIS aliyekaa upande wa Kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika la OXFAM,Tanzania Bi MONICA GORDON.


STEVEN KANUMBA kushoto akiwa pamoja na KRISTIN DAVIS mara baada ya Uzinduzi wa Nembo ya Shindano la Mama Shujaa wa Chakula katika Kijiji cha Makumbusho Jijini Dar es Salaam.

Mcheza Filamu na Balozi wa Kampeni ya Grow inayoratibiwa na Shirika la OXFAM hapa nchini STEVEN KANUMBA akicheza Ngoma mara baada ya Uzinduzi wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula Jijini Dar es Salaam.