Wednesday, December 28, 2011

* Dakta Ali Shein ahudhuria mazishi ya kanal Nassor Waziri Mageta


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dkt ALI MOHAMMED SHEIN (wa tatu kulia) pamoja na Viongozi wengine wakiusalia mwili wa Marehemu Kanal NASSOR WAZIRI MAGETA aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Valantia katika msikiti wa masjid Twariq Bububu nje wa mji wa Zanzibar, aliyefariki jana na kuzikwa Kijijini kwao Mkanyageni Wilaya ya Magharibi Unguja.


Askari wa Vikosi vya SMZ wakilibeba Jeneza lenye mwili waMarehemu Kanal NASSOR WAZIRI MAGETA aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Valantia.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza laMapinduzi Alhaj Dkt ALI MOHAMMED SHEIN akitia udongo katika kaburi la Marehemu Kanal NASSOR WAZIRI MAGETA.


Askari wa Vikosi vya SMZ wakitoa salamu ya hesha katika kaburi la marehemu Kanali NASSOR WAZIRI MAGETA aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Valantia.

No comments:

Post a Comment