Sunday, May 13, 2012

Msanii wa Filamu za Kitanzania Juma Kilowoko"Sajuki" amepelekwa nchini India kwa Ajili ya Matibabu

Mwana-Filamu JUMA KILOWOKO "Sajuki" akiwa katika picha mbili tofauti, kulia ni mkewe WASTARA JUMA

Mwana-Filamu Mahiri hapa nchini JUMA KILOWOLO anayejulikana kama SAJUKI katika tasnia uigizaji,amepelekwa INDIA kwa ajili ya kufanyiwa Oparesheni ya kuondolewa uvimbe tumboni, ambapo kwa mujibu wa madaktari nchini humo wanadai kwamba upo karibu na INI.
SAJUKI ameondoka leo katika uwanja wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere akiambatana na mkewe WASTARA JUMA ambae pia ni Mwana-Filamu, hii ni mara ya Pili kupelekwa nchini INDIA ambapo awali alienda kwa lengo la kufanyiwa vipimo vya damu.
Kuondoka kwa SAJUKI kunafuatia Juhudi mbalimbali zilizofanywa na wasanii wa filamu pamoja wadau wengine wa tasnia hiyo wakiwemo viongozi wa juu wa Serikali.
Dua za Watanzania Bado zinahitajika kumuombea kwa mwenyezi mungu Mwana-Filamu SAJUKI ili aweze kutibiwa na kupona na hatimae arejee nchini kuendelea na majukumu yake ya Ujenzi wa Taifa……Ameein.
                                                            
                                               

No comments:

Post a Comment