Wednesday, November 30, 2011

* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Bilal afunga mkutano wa nchi za maziwa makuu mjini Bujumbura


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Burundi Dkt JAMES MWASI baada ya kuwasili kwenye ukumbi wa Golf kwa ajili ya kufunga Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu, uliokuwa ukijadili Uendelezwaji wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED BILAL akisoma hotuba yake ya kufunga Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu.


Waziri wa Afrika Mashariki, SAMUEL SITTA akiwa katika Ukumbi wa Golf akimsikiliza kwa makini Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED BILAL alipokuwa akifunga rasmi Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu uliokuwa ukijadili Uendelezwaji wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika uliomalizika mjini Bujumbura nchini Burundi.

Monday, November 28, 2011

* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Bilal afungua Mkutano wa Viongozi wa Takukuru Mkoani Tanga


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Viongozi wa Takukuru Mkoani Tanga Kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Takukuru, EDWARD HOSEA kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga CHIKU GALAWA na waziri wa Ofisi ya Rais-Utawala Bora, MATHIAS CHIKAWE.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED BILAL akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Takukuru, EDWARD HOSEA mara baada ya kufungua rasmi mkutano Mkuu wa Viongozi wa Takukuru.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED BILAL akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Takukuru, EDWARD HOSEA wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Viongozi wa Takukuru, uliofanyika Mkoani Tanga Kushoto ni waziri wa Ofisi ya Rais- Utawala Bora, MATHIAS CHIKAWE.


Baadhi ya Wakuu wa Vitengo wa Takukuru waliohudhuria Mkutano huo Mkuu wa Mwaka ulioanza leo Novemba 28 na kumalizika kesho, Mkoani Tanga.

Saturday, November 26, 2011

* Mwakilishi wa UNDP amaliza muda wake wa kazi hapa nchini


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la mapinduzi Dkt ALI MOHAMMED SHEIN akisalimiana na mwakilishi wa Shirika la maendeleo la umoja wa mataifa UNDP anayeishi Visiwani humo, SORO KARNA aliyefika Ikulu ya Mjini Zanzibar kumuaga Rais baada ya kumaliza muda wake wa Kazi hapa nchini.

Rais wa Zanzibar Dkt ALI MOHAMMED SHEIN akizungumza na mwakilishi wa UNDP Bwana SORO KARNA aliyefika Ikulu ya Mjini Zanzibar kumuaga Rais.

* Makamu wa Rais Dakta Gharib Bilal azindua Tamasha la utamaduni wa Mtanzania


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa tamasha la Siku ya Utamaduni wa Mtanzania iliyowasilishwa na Kabila la Jamii za Mikoa ya Rukwa na Katavi lililofanyika kwenye Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akitoka ndani ya nyumba ya asili ya watu wa Kabila la Wafipa baada ya uzinduzi wa tamasha la Siku ya Utamaduni wa Mtanzania ndani ya kijiji cha Makumbusho.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akimsikiliza Waziri Mkuu MIZENGO PINDA wakati akimpa maelezo kuhusu kinywaji cha kienyeji Pombe ya Chimpumu inayotumiwa na Kabila la watu wa Rukwa.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akimshuhudia Waziri Mkuu MIZENGO PINDA akinywa kinywaji cha asili aina ya Chimpumu ‘Pombe ya Isute’ kinachotengenezwa na Kabila la watu wa Katavi na Rukwa wakati wa uzinduzi wa Tamasha la Siku ya Utamaduni wa Mtanzania iliyowasilishwa na na Kabila la Jamii za Mikoa ya Rukwa na Katavi lililofanyika kwenye Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam.

* Mahafali ya Pili ya Chuo kikuu cha Dodoma UDOM yafana


Kiongozi wa timu ya Viongozi wa Juu wa UDOM wakiwa katika Maandamano ya kuelekea kwenye Mahafali ya Chuo Kikuu cha Dodoma.


Baadhi ya Viongozi chuo kikuu cha Dodoma wakiwa tayari kwenye Maandamano kuelekea kwenye Mahafali ya Pili ya chuo hicho.


Viongozi wa chuo kikuu cha Dodoma wakiongozwa na Mkuu wa chuo hicho Rais Mstaafu wa awamu ya tatu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, BENJAMIN WILLIAM MKAPA wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa unaimbwa katika Mahafali ya Chuo Kikuu Cha Dodoma UDOM


Baadhi ya wahitimu wa Shahada ya kwanza ya Sosholojia wakiwa katika furaha Mara baada ya kutunukiwa Shahada zao.

Friday, November 25, 2011

* Kampuni ya Tigo Tanzania yakabidhi Majengo ya madarasa mawili kwa Shule ya Msingi ya Pugu kajiungeni


Mwakilishi wa kampuni ya Tigo ALEX MSIGARA akiongea na wanafunzi wa Shule ya Msingi Pugu Kajiungeni wakati wa kukabidhi madarasa jijini Dar es Salaam, Kulia kwake ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bi. MARIAM KORONGO, kushoto kwake ni Afisa Elimu, Vifaa na Takwimu (W) Ilala ABILAH MCHIA.


Afisa Elimu, ABILAH MCHIA akizungumza na waandishi wa habari na walimu wakati kampuni ya Tigo ilipokuwa ikikabidhi  madarasa mawili ya Shule ya Msingi Pugu Kajiungeni jijini Dar Es Salaam, Kulia kwake ni mwakilishi wa Tigo ALEX MSIGARA na mwalimu mkuu Bi. MARIAM KORONGO.


Mwakilishi wa kampuni ya Tigo, ALEX MSIGARA akimkabidhi mwalimu mkuu wa shule ya msingi Pugu Kajiungeni Bi MARIAM KORONGO madaftari, kalamu za Tigo pamoja na T-shirt.

Tigo yakabidhi madarasa mawili

Tarehe 22 November 2011, Dar es Salaam, Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo  imekabidhi madarasa mawili kwa shule ya msingi Pugu Kajiungeni iliyopo eneo la Gongolamboto jijini Dar es salaam baada ya kumaliza ukarabati wa majengo ya shule hiyo yaliyoharibiwa na mlipuko wa mabomu yaliyolipuka katika kambi ya Gongolamboto mwezi May jijini Dar es Salaam.

Akizungumza mara baada ya kukabithi rasmi majengo hayo kwa mwalimu mkuu wa shule hiyo, Afisa viwango na mwakilishi wa kampuni ya simu za mikononi ya Tigo Alex Msigara amesema “Sisi kama kampuni ya simu za mikononi ya Tigo tuliguswa kwa namna ya kipekee na tukio hili hasa ukichukulia kuwa wahanga wakubwa walikuwa ni watoto ambao walitaharuki na kuanza kukimbia huku na huko, na wengine kushindwa kwenda shule kutokana na mjengo kuharibika hali iliyowaondolea amani wakiwa shule”

Alex akaongeza “Nadhani waandishi na wananchi wanaoipenda Tigo watakuwa ni mashahidi kuwa sisi tumekuwa mstari wa mbele katika kuchangia elimu hasa elimu ya msingi ambapo tumeweza kutoa vitabu na vibao vya mapajani siku chache zilizopita kwa baadi ya shule za msingi nchini kwani tunaamini watoto wakikua katika misingi yenye yenye uelekeo mzuri kielimu basi wao ndio watakaoijenga Tanzania nzuri siku za usoni”

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Pugu Kajiungeni Bi Mariam Korongo akitoa shukrani zake kwa Tigo amesema “kwa niaba ya walimu, wazazi wa wanafunzi na wanafunzi wenyewe wa shule ya msingi Pugu Kajiungeni, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa msaada huu wa kutengenezewa madarasa haya mawili. Tunashukuru kuona kwamba taasisi binafsi zinakuwa zinaguswa na matatizo yanayozikumba jamii inayozizunguka kwani hiyo inapunguza mzigo kwa serikali ambayo inafanya juhudi kubwa katika kuhakikisha inaleta maendeleo nchini.”

Mwalimu mkuu akaongeza pia kuwa anafurahi kwamba Tigo wameweza kuwasaidia katika tatizo hilo la ukarabati wa majengo na kuziomba taasisi nyingine kuchangia sekta ya elimu katika shule mbalimbali kwani matatizo yanafanana nchini kote.

Mara baada ya tukio la mlipuko wa mabomu familia za maeneo yale zilipata misukosuko mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupotezana kwa hofu, kuharibika kwa makazi na maeneo ya biashara, Tigo ilitembelea maeneo yale na kujionea jinsi uharibifu ulivyotokea na kuwapa mkono wa pole wahanga na namna ya pekee ikiwa ni pamoja na kuchukua jukumu la kukarabati majengo ya shule yaliyoharibiwa.

Tuesday, November 22, 2011

Kikao cha kamati kuu CC ya chama cha Mapinduzi CCM kinaendelea Mjini Dodoma



Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa wa chama hicho wakisubiri kuanza kwa kikao ambacho kinaingia siku ya pili mjini Dodoma.

* Benki ya NIC Tanzania yadhamini mchezo wa Gofu ili kusaidia watu wenye uoni hafifu nchini


Mkurugenzi na Mtendaji Mkuu wa Benki ya NIC Tanzania, JAMES MUCHIRI (kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Meneja Mikopo wa benki hiyo Bi REGINA MWENGI , PRISCILLA KAROBIA na DAVID MUTHUNGU kabla ya kuanza kwa michuano ya gofu iliyoandaliwa na Lions Club na kufanyika kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam, Benki hiyo ilidhamini kiwanja namba kumi kwa shilingi Milioni 3.5.


PRISCILLA KAROBIA ambaye ni mmoja ya wanachama wa Klabu ya Gymkhana akiangalia mpira baaada ya kuupiga wakati wa Mashindano ya Gofu yaliyofanyika katika Viwanja vya Gymkhana ili kusaidia watu wenye matatizo ya kuona.


Mkurugenzi na Mtendaji Mkuu wa Benki ya NIC Tanzania, JAMES MUCHIRI akiangalia mpira baaada ya kuupiga wakati wa Mashindano ya Gofu yaliyofanyika katika Viwanja vya Gymkhana ili kusaidia watu wenye matatizo ya kuona ambapo benki hiyo ilidhamini kiwanja namba kumi kwa shilingi Milioni 3.5.


Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya NIC Tanzania akiwemo Mkurugenzi na Mtendaji Mkuu wa Benki ya NIC Tanzania, JAMES MUCHIRI (Katikati) wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wanachama Lions Club wakati wa michuano ya Gofu iliyofanyika kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam ili kusaidia watu wenye matatizo ya macho.

Benki NIC Tanzania yajitosa kudhamini Gofu kusaidia wenye uoni hafifu

Na Mwandishi Wetu

Benki ya NIC Tanzania kwa kushirikiana na Klabu ya Lions ya Jijini Dar es Salaam wamejitokeza kudhamini mashindano ya mchezo ya Gofu ili kusaidia watu wenye matatizo ya macho.

Katika mashindano hayo benki hiyo imetoa jumla ya Dola za Kimarekani 2000 sawa na Shilingi Milioni 3.5 za Tanzania lengo likiwa ni kuinua afya za wananchi hususani wanaosumbuliwa na matatizo ya macho.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mashindano hayo yaliyoshirikisha wachezaji zaidi ya 105, Mkurugenzi na Mtendaji Mkuu wa NIC Bank Tanzania James Muchiri amesema ni matarajio yao kwamba udhamini huo utasaidia upatikanaji wa afya bora katika eneo wanalotoa huduma zake.

“Tunatarajia msaada huu ambao ni wa kwanza katika sekta hii ya michezo kupitia Lions Club utasaidia watu wenye matatizo wa macho katika maeneo watakayoenda kutoa huduma hiyo kama ilivyo kawaida ya wana Mzizima,” alisema Muchiri.

Mbali na hayo Mkurugenzi na Mtendaji huyo Mkuu wa NIC Bank Tanzania alisema inakadiwa kuwa zaidi ya watu milioni tatu nchini wanakabiliwa na upofu kutyokana na uwezo mdogo wa kifedha, miongoni mwao wakiwemo wanafunzi.

Kutokana na hilo alisema watahakikisha wanajenga uhusiano mzuri baina yao na Lions Club katika kuunga mkono mchezo wa gofu na kuwahudumia wenye matatizo ya macho.

Nchini Benki hiyo ina matawi Harbour View Tower jijini Dar es Salaam, Mwanza and Arusha huku ikitoa huduma mbalimbali ikiwemo mikopo yenye riba nafuu.

* Benki ya KCB Tanzania yakabidhi vitabu vya somo la Sayansi vyenye thamani ya Shilingi milioni 1.5 kwa Sekondari ya Kangaye Jijini Mwanza


Meneja wa KCB Tanzania tawi la Mwanza ELIAS MWAKATOBE akimkabidhi Afisa Elimu Sekondari Jiji la Mwanza ANNE ALOPA baadhi ya vitabu vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.5 vilivyotolewa na benki hiyo kwa shule ya sekondari ya Kangaye wakati wa hafla iliyofanyika Nyamagana jijini Mwanza hivi karibuni.


Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mahusiano wa KCB Tanzania Bi CHRISTINE MANYENYE akimkabidhi Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kangaye JOSEPHINE MLUNDWA baadhi ya vitabu vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.5 vilivyotolewa na benki hiyo wakati wa hafla iliyofanyika Nyakato jijini Mwanza hivi karibuni, anayeshuhudia katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo JOSEPH NYANDA.


Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mahusiano wa KCB Tanzania Bi CHRISTINE MANYENYE akiwakabidhi kaka mkuu wa shule ya sekondari Kangaye MARWA MANG'ANA, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kangaye JOSEPHINE MLUNDWA na dada mkuu GRACE GIMAHENGA baadhi ya vitabu vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.5 vilivyotolewa na benki hiyo wakati wa hafla iliyofanyika Nyamagana jijini Mwanza.


Wanafunzi wa kidato cha tatu wa shule ya Sekondari Kangaye iliyopo Nyamagana jijini Mwanza wakifanya mazoezi ya maabara ki-vitendo wakati Benki ya KCB Tanzania ilipokabidhi msaada wa vitabu vya sayansi wenye thamani ya shilingi Milioni 1.5 hivi karibuni.


KCB Tanzania yaomba wanafunzi wawezeshwe ubunifu

Na Mwandishi wetu, Mwanza

Benki ya KCB Tanzania imeiomba serikali kuongeza vifaa vya kufundishia katika shule mbalimbali nchini ili kuwawezesha walimu nchini kuibua vipaji tofauti vya ubunifu walivyonavyo wanafunzi.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mahusiano wa KCB Tanzania Bi Christine Manyenye hivi karibuni wakati akikabidhi msaada wa vitabu vya masomo ya Sayansi vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.5 kwa shule ya Sekondari Kangaye iliyopo Nyamagana jijini Mwanza.

Akifafanua Manyenye alisema kuwa kutokana na mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia wanafunzi wengi wameonesha utayari kubuni vitu mbalimbali lakini wanashindwa kuendelea mbele kwa kukosa miongozo ya kufika watakapo.

Vilevile aliongeza kuwa msaada huo wa vitabu vilivyotolewa na KCB Tanzania utawezesha wanafunzi wa Sekondari ya Kangaye kujifunza masuala mbalimbali yatakayowasaidia kubuni bidhaa mbalimbali ambazo sasa zinaagizwa kutoka nje ya nchi.

“Hivi sasa hata kalamu za kuandikia zinaingizwa kutoka nje, hili linasababishwa na wanafunzi kutowezeshwa kuwa wabunifu tangu wakiwa watoto. KCB Tanzania imeliona hili na kuamua kuwekeza katika kusaidia vitabu hivi vya kisayansi ili kukuza uelewa miongoni mwao,” Alisema Manyenye.

Kwa upande wake Afisa Elimu wa Shule za Sekondari Jiji la Mwanza Anne Alopa alisema shule nyingi nchini zinakabiliwa na upungufu wa vifaa vya kiada licha ambapo serikali imekuwa ikijitahidi kulipatia ufumbuzi suala hilo.

Kutokana na hilo Alopa alitumia fursa hiyo kuipongeza Bodi ya Shule ya Sekondari Kangaye kwa kumtafuta mdhamini huyo ambaye tayari ameonesha nia ya kuendelea kuisaidia shule hiyo baada ya awali kujitokeza kupanda miti zaidi ya 3,000 shule hapo.

“Naipongeza KCB Tanzania kwa kuanza kutekeleza ahadi zake za kuisaidia Kangaye, natoa wito kwa uongozi wa shule kuendelea kushirikiana na benki hii ili kuweza kupata misaada zaidi,” alisema Afisa Elimu huyo.

Naye Mkuu wa Shule hiyo Josephine Mlundwa alisema msaada huo wa vitabu kutoka benki hiyo umepunguza mahitaji kwa asilimia 30 na kwamba utawezesha walimu kuongeza kiwango cha ufundishaji kwa wanafunzi.

Mbali na hayo alizitaja changamoto nyingine zinazoikabili shule hiyo kuwa ni umeme, maji, vifaa vya maabara, viti na meza za maabara na za walimu, majengo ya utawala, maktaba, vyoo, nyumba za walimu, maabara kwani sasa wanatumia vyumba vya madarasa kama maabara kwa kufundishia masomo ya Sayansi.

Saturday, November 19, 2011

* Wanachuo UDOM wafanya Kongamano kujadili kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania.


Mwendesha Mada CHARLES MUHONI akitoa ufafanuzi juu ya Shilingi ya Tanzania Kwanini inaporomoka kila siku katika kongamano lililofanyika katika ukumbi wa kufundishia wa chuo kikuu cha Dodoma UDOM.


Mwanafunzi anayesoma Shahada ya Uchumi FIDELIS MROSSO akifafanua juu ya Maswala mazima ya Shilingi ya Tanzania dhidi ya Pesa za kigeni hasa Dola ya Marekani.

Mwanafunzi anayesomea masuala ya Uchumi, ZAHARA MUHIDIN akichangia Mada wakati wa Kongamano hilo.


Baadhi ya Wanafunzi walioshiriki Kongamano hilo lililofanyika katika Chuo Kikuu Cha Dodoma UDOM.

Friday, November 18, 2011

* Balozi wa kinywaji cha Hennessy awaeleza wanahabari kuhusu maajabu ya Hennessy XO


Balozi wa kinywaji cha Hennessy Bwana CYRILLE GAUTIER'S anayeishi katika ubingwa wa dunia ya maajabu ya Hennessy nchini Ufaransa akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akielezea juu ya kinywaji cha Hennessy.


Balozi wa Hennessy Bwana CYRILLE GAUTIER'S akiwaonyesha waandishi wa Habari (hawapo pichani) aina ya kinywaji cha Hennessy XO kinachotengenezwa nchini Ufaransa na kusambazwa kote Barani Afrika.

* Mke wa makamu wa Rais wa Tanzania Mama Asha Bilal ahudhuria maadhimisho ya miaka 50 ya taasisi ya Alliance Francaise.


Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama ASHA BILAL akisoma Hotuba yake wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Taasisi ya Alliance Francaise Jijini Dar es Salaam Tanzania,.iliyofanyika katika Ukumbi wa Alliance Francaise, Katikati ni Balozi wa Ufaransa hapa nchini, MARCEL ESCURE,kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, JULIA GIANNETTI.


Mke wa Makamu wa Rais Mama ASHA BILAL akizungumza jambo na Balozi wa Ufaransa, MARCEL ESCURE, wakati alipokuwa mgeni rasmi katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Taasisi ya Alliance Francaise.

Tuesday, November 15, 2011

* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Bilal apokea madai ya wanaharakati kuhusu mabadiliko ya Tabia Nchi


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akipokea Madai ya Wananchi ya Namna ya kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia nchi kutoka kwa Mwanaharakati wa Mabadiliko ya tabia Nchi LAWRENCE CHUMA wakati wa Kongamano la Msafara wa kuelekea katika Mkutano wa Mabadiliko ya Tabia Nchi unaotarajia kufanyika Durban, Afrika Kusini mwezi ujao.


Makamu wa Rais, Dkt MOHAMMED BILAL akizungumza wakati wa Kongamano la Msafara wa kuelekea katika mkutano wa mabadfiliko ya Tabia Nchi utakaofanyika Durban, Afrika Kusini.

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Shein akutana na wataalam wa Sekta ya Maji


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt ALI MOHAMMED SHEIN akizungumza na wataalam wanaohusiana na sekta ya maji walipofika katika ukumbi wa mikutano wa jumuiya ya wafanya biashara, (kulia) ni Mel STEWART OBE, na PETER JACKSON,mazungumzo hayo yalifuatia baada ya makubaliano yaliyofanyika na Rais wa Zanzibar na Kiongozi wa Sharjah Sheikh Sultan MOHAMMED Al QASIMI, juu ya mashirikiano katika vyanzo vya maji safi na salama Zanzibar.

Sunday, November 13, 2011

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Shein atembelea kampuni ya Vifaa vya Ujenzi Huko Ras Al Khaimah


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt ALI MOHAMMED SHEIN, akizungumza na Sheikh SAUD Bin SAQR Al QASIMI ambae ni Mwenyeji wake na Kiongozi wa Ras Al Khaimah,wakati alipowasili katika kasri ya kiongozi huyo akiwa katika ziara ya kukuza uhusiano wa Ki-maendeleo katika sekta mbali mbali.


Rais wa Zanzibar  Dkt ALI SHEIN akikaribishwa na Naibu Mtendaji Mkuu wa kampuni ya ujenzi ya Rak Ceramics, Bwana ABDALLAH MASSAAD,wakati alipotembelea kuona vifaa mbali mbali vya ujenzi huko Ras Al Khaimah,akiwa katika ziara ya kukuza uhusiano na mashirikiano katika sekta za maendeleo.


Rais wa Zanzibar Dkt ALI  SHEIN akitembelea pamoja na kupata maelezo kutoka kwa Naibu Mtendaji Mkuu wa kampuni ya ujenzi ya Rak Ceramics ABDALLAH MASSAAD huko Ras Al Khaimah.

Friday, November 11, 2011

* Rais Dakta Jakaya Kikwete afunga mkutano wa uwekezaji katika Sekta ya Kilimo


Rais Dkt JAKAYA KIKWETE akifunga Mkutano wa Kazi uliojadili Mpango wa Uwekezaji Katika Sekta ya Kilimo na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta hiyo wakiwemo mabalozi zaidi ya 15, wawakilishi wa taasisi za kimataifa, Mawaziri na Viongozi kadhaa kutoka Serikalini pamoja na wadau wa sekta ya umma.


Rais Dkt JAKAYA KIKWETE akizungumza na wadau wa maendeleo baada ya kufunga Mkutano wa Kazi uliojadili Mpango wa Uwekezaji Katika Sekta ya Kilimo na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta hiyo.

* Rais Dakta Jakaya Kikwete ahudhuria mkutano wa majadiliano ya Sekta Binafsi na Umma


Rais Dkt JAKAYA KIKWETE akihutubia mkutano wa majadiliano ya sekta za umma-na-binafsi katika kusawazisha uwiano wa kodi kwa nchi za Afrika Mashariki ambao umefanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Benki kuu ya Tanzania.


Rais Dkt JAKAYA KIKWETE akiwasili katika ufunguzi wa majadilino ya sekta za umma-na-binafsi, huku akisindikizwa na Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki SAMWEL SITTA.