Sunday, August 28, 2011

* Rais Jakaya Kikwete ahudhuria futari iliyoandaliwa na Makamu wake Dakta Mohammed Gharib Bila katika makazi yake OYSTERBAY Jijini Dar es Salaam


Rais Dakta JAKATA KIKWETE, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL, Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti ISSA SHAABAN SIMBA na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad MUSSA SALUM, wakisubiri muda wa swala kabla ya kupata futari iliyoandaliwa na Makamu wa Rais katika makazi yake Oysterbay jijini Dar es Salaam.


Rais Dakta JAKAYA KIKWETE, Makamu wake Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, SAID MECK SADICK, wakiomba dua kwa pamoja baada ya kupata futari iliyoandaliwa na mwenyeji wao Makamu wa Rais Dakta BILAL
 

Wednesday, August 24, 2011

* Viongozi wa Kitaifa wahudhuria Mazishi ya aliyekuwa mwakilishi wa Jimbo la Uzini Unguja, Mussa Hamis Silima aliyefariki kwa ajali ya Gari Mkoani Dodoma


Rais wa Zanzibar, Dakta ALI MOHAMMED SHEIN, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL, Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim SEIF SHARIFF HAMAD pamoja na baadhi ya viongozi wakiwa katika dua ya kumuombea aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Unguja, marehemu MUSSA HAMIS SILIMA aliyefariki Agosti 23 katika hospitali ya Muhimbili Dar es Salaam, alikolazwa baada ya kupata ajali Agosti 22.


Makamu Wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta  MOHAMMED GHARIB BILAL akishiriki na baadhi ya Viongozi, kubeba Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Uzini, marehemu MUSSA HAMIS SILIMA, wakati wa shughuli za maziko zilizofanyika katika Kijiji cha Kiboje Wilaya ya Kati Unguja.



Tuesday, August 23, 2011

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Mohammed Shein akutana na Uongozi wa Wizara ya Katiba na Sheria ya Zanzibar



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dakta ALI MOHAMMED SHEIN akizungumza na uongozi wa Wizara ya katiba na Sheria, Ikulu Mjini Zanzibar katika mfululizo wa kuzungumza na kila uongozi wa wizara Visiwani humo.

Monday, August 22, 2011

* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Gharib Bilal amuaga rasmi Balozi wa Misri anayemaliza muda wake Wael Adel Nasr


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akizungumza na Balozi wa Misri anayemaliza muda wake hapa nchini WAEL ADEL NASR aliyefika ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam kwa ajili ya kumuaga rasmi.


Makamu wa Rais wa Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL pamoja na Balozi wa Misri anayemaliza muda wake WAEL ADEL NASR aliyefika ofisini kwake Ikulu, Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumuaga, Kushoto ni Msaidizi wa Balozi huyo AMR MAHMOUD.

Sunday, August 21, 2011

* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Gharib Bilal ahudhuria Fainali za Mashindano ya Kuhifadhi Qur'an yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL pamoja na Rais Mstaafu wa awamu ya pili,  Alhaj ALI HASSAN MWINYI wakiwa katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam wakifuatilia kwa makini fainali za mashindano ya kuhifadhi Qur-an.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akisoma Hotuba yake wakati wa fainali za mashindano ya kuhifadhi Qur-an, yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam na kushirikisha jumla ya washiriki 14 kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kati.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akimkabidhi zawadi mshindi wa kwanza wa fainali za mashindano ya kuhifadhi Qur-an JAHUDDIN ADAM kutoka Sudan mara baada ya kutangazwa mshindi wa fainali hizo zilizofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL, Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Alhaj ALI HASSAN MWINYI pamoja na baadhi ya Viongozi wa dini ya Kiislamu wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa fainali za mashindano ya kuhifadhi Qur-an, baada ya kumalizika kwa mashindano hayo katika ukumbi wa Diamond Jubilee.

Friday, August 19, 2011

* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Gharib Bilal asaini kitabu cha Makubaliano ya Mkutano wa 31 wa SADC uliofanyika mjini Luanda nchini ANGOLA.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakat MOHAMMED GHARIB BILAL akisaini kitabu cha maafikiano yaliyotokana kuhusu itifaki ya pamoja kwa nchi za SADC inayohusu udhibiti wa fedha chafu sambamba na katiba ya ushirikiano wa majeshi ya Polisi kwa nchi wanachama yaliyoafikiwa katika mkutano wa 31 wa Viongozi wa Mataifa ya SADC mjini Luanda Angola.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akisalimiana na Waziri Mkuu wa Zimbabwe, MORGAN TSVANGIRAI walipokutana kwenye mkutano wa 31 wa Viongozi wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC.

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, BERNARD MEMBE pamoja na Wajumbe kutoka nchi mbalimbali za Jumuiya ya Maendeleo zilizopo kusini mwa Afrika wakiwa katika mkutano wa 31 wa Viongozi wa Jumuiya hiyo uliomalizika nchini Angola Agosti 18, 2011.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akikagua Gwaride lililoandaliwa maalum kwa ajili ya kumuaga wakati alipokuwa akiondoka uwanja wa ndege wa Fevereiro uliopo jijini Luanda, Angola baada ya kumalizika kwa mkutano wa 31 wa Viongozi wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC

Wednesday, August 17, 2011

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Mohammed Shein azungumza na Watendaji wa Wizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo Visiwani humo



Rais wa Zabziar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dakta ALI MOHAMMED SHEIN akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Habari, Utalii ,Utamaduni na Michezo, katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar, Ikiwa ni mfululizo wa ratiba zake za kuzungumza na kila Wizara,katika kuhakikisha taasisi za wizara hizo zinatekeleza majukumu yake.



Tuesday, August 16, 2011

* Wananchi wa Vijiji vitano katika wilaya ya Bagamoyo kufaidika na mradi wa visima


Kutoka kushoto ni BERTHA IKUA wa kampuni ya Spear head Africa Dakta SALIM ABDULLA Mkurugenzi wa Taasisi ya Afya ya Ifakara pamoja na NARCISIUS NGAILLO ambae ni meneja mauzo wa kampuni ya Vinywaji ya Tanzania Distillers Limited wakizungumza na waandishi wa Habari kuhusu kuanza kwa mradi wa uchimbaji wa Visima takribani 6 katika vijiji vitano vilivyopo wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani ambavyo vitagharimu kiasi cha Shilingi milioni 42.

* Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad atembelea maghala ya kuhifadhia Karafuu kisiwani Pemba


Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim SEIF SHARIFF HAMAD akiangalia karafuu zilizochakachuliwa kwa pamoja na unga wa makonyo, mchanga pamoja na maji katika Ghala la kuhifadhia karafuu Mkoani kisiwani Pemba,Kulia kwake ni Meneja Mkuu wa ZSTC HAMAD KHAMIS HAMAD na kushoto ni Mkuu wa Kusini Pemba JUMA KASSIM TINDWA.

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Mohammed Shein afuturisha Wananchi wa kijiji cha Mkanyageni Mkoa wa Kusini Pemba


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Alhaj Dakta ALI MOHAMMED SHEIN akisalimiana na Mtoto MUSSA MAKAME BADRU wa kijiji cha Mkanyageni Mkoa wa Kusini Pemba baada ya kufutari pamoja na wazee hao katika futari maalum aliyowaandalia katika viwanja vya Skuli ya Mkanyageni.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Alhaj Dakta ALI MOHAMMED SHEIN akiwa katika futari na wananchi na wazee wa kijiji cha Mkanyageni Mkoa wa Kusini Pemba aliyowaandalia katika viwanja vya Skuli ya Mkanyageni.




* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Gharib Bilal azindua Ujenzi wa Maghorofa 30 ya Kambi ya Jeshi la Polisi Barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akikata utepe kuzindua Maghorofa 30 ya Kambi ya Polisi yaliyopo Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, SHAMSI VUAI NAHODHA (kulia) ni Inspekta Jenerali wa Polisi, SAID MWEMA.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akisikiliza maelezo kutoka kwa msimamizi wa Mradi wa ujenzi wa Maghorofa 30 ya Kambi ya Polisi, Dakta HUBA NGULUMA.
 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, SHAMSI VUAI NAHODHA akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi huo.


Baadhi ya maofisa wa jeshi la Polisi waliohudhuria hafla hiyo ya uzinduzi, wakisikiliza kwa makini Hotuba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL.





Tuesday, August 9, 2011

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Mohammed Shein kwa nyakati tofauti amekutana na Balozi wa Nigeria nchini pamoja na Viongozi wa Jumuiya ya Mabohora Zanzibar


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dakta ALI MOHAMMED SHEIN akizungumza na Balozi wa Nigeria nchini Tanzania Dakta ISHAYA SAMAILA MAJANBU alipofika Ikulu Mjini Zanzibar.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dakta ALI MOHAMMED  SHEIN akisalimiana na Balozi wa Nigeria Dakta ISHAYA SAMAILA MAJANBU kabla ya kuanza mazungumzo yao.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dakta ALI MOHAMMED SHEIN akisalimiana Viongozi wa jumuiya ya Mabohora Zanzibar, wakiongozwa na Mwenyekiti AAMIL SAHEB SHEIKH SHABBIR ISMAIL walipofika Ikulu Mjini Zanzibar kuonana nae.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dakta ALI MOHAMMED SHEIN akizungumza na Viongozi wa Jumuiya ya Mabohora Zanzibar, walipofika Ikulu Mjini Zanzibar.


Monday, August 8, 2011

* Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu na Bunge William Lukuvi atembelea Banda la Mamlaka ya Hali ya Hewa


Mheshimiwa WILLIAM LUKUVI akipata maelezo kutoka kwa mtaalamu wa hali ya hewa Mkurugenzi wa Utafiti Dakta E. MPETA, pembeni ni afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo MONICA MUTONI,akifuatilia kwa karibu, katika banda la Mamlaka hiyo ndani ya Viwanja vya Nanenane mkoani Dodoma.