Wednesday, August 24, 2011

* Viongozi wa Kitaifa wahudhuria Mazishi ya aliyekuwa mwakilishi wa Jimbo la Uzini Unguja, Mussa Hamis Silima aliyefariki kwa ajali ya Gari Mkoani Dodoma


Rais wa Zanzibar, Dakta ALI MOHAMMED SHEIN, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL, Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim SEIF SHARIFF HAMAD pamoja na baadhi ya viongozi wakiwa katika dua ya kumuombea aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Unguja, marehemu MUSSA HAMIS SILIMA aliyefariki Agosti 23 katika hospitali ya Muhimbili Dar es Salaam, alikolazwa baada ya kupata ajali Agosti 22.


Makamu Wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta  MOHAMMED GHARIB BILAL akishiriki na baadhi ya Viongozi, kubeba Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Uzini, marehemu MUSSA HAMIS SILIMA, wakati wa shughuli za maziko zilizofanyika katika Kijiji cha Kiboje Wilaya ya Kati Unguja.



No comments:

Post a Comment