Friday, August 19, 2011

* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Gharib Bilal asaini kitabu cha Makubaliano ya Mkutano wa 31 wa SADC uliofanyika mjini Luanda nchini ANGOLA.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakat MOHAMMED GHARIB BILAL akisaini kitabu cha maafikiano yaliyotokana kuhusu itifaki ya pamoja kwa nchi za SADC inayohusu udhibiti wa fedha chafu sambamba na katiba ya ushirikiano wa majeshi ya Polisi kwa nchi wanachama yaliyoafikiwa katika mkutano wa 31 wa Viongozi wa Mataifa ya SADC mjini Luanda Angola.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akisalimiana na Waziri Mkuu wa Zimbabwe, MORGAN TSVANGIRAI walipokutana kwenye mkutano wa 31 wa Viongozi wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC.

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, BERNARD MEMBE pamoja na Wajumbe kutoka nchi mbalimbali za Jumuiya ya Maendeleo zilizopo kusini mwa Afrika wakiwa katika mkutano wa 31 wa Viongozi wa Jumuiya hiyo uliomalizika nchini Angola Agosti 18, 2011.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akikagua Gwaride lililoandaliwa maalum kwa ajili ya kumuaga wakati alipokuwa akiondoka uwanja wa ndege wa Fevereiro uliopo jijini Luanda, Angola baada ya kumalizika kwa mkutano wa 31 wa Viongozi wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC

No comments:

Post a Comment