Tuesday, January 31, 2012

* Balozi wa Marekani hapa nchini, Alfonso Lenherts akutana na Rais wa Zanzibar Dakta Ali Shein katika Ikulu ya mjini Unguja


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt ALI MOHAMMED SHEIN akisalimiana na Balozi wa Marekani Nchini Tanzania ALFONSO LENHERTS alipofika Ikulu Mjini Zanzibar.



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt ALI MOHAMMED SHEIN akizungumza na Balozi wa Marekani Nchini Tanzania ALFONSO LENHERTS alipofika Ikulu Mjini Zanzibar na ujumbe wake.

* President Jakaya Kikwete hands over ALMA chair to President Ellen Johnson Sirleaf of Liberia


President JAKAYA KIKWETE makes his opening speech and give the status of Malaria, Others from left is the new AU Chairman President of Benin, the Executive Secretary of ALMA, Ms JOY PHUMAPHI, new ALMA Chair and President of Liberia Madame ELLEN JOHNSON SIRLEAF, and newly elected ALMA Vice Chair and President of Mozambique, Mr ARMANDO GUEBUZA.


New ALMA Chair President ELLEN JOHNSON SIRLEAF confers to out-going chair President JAKAYA KIKWETE an award of Excellence from the UN Secretary General and the African Union Chairman for sound policies and effort to combating malaria.


Across section of African Leaders Malaria Alliance ALMA leaders at the working session luncheon at the Africa Union Summit during which out-going Chairman President JAKAYA KIKWETE handed over the ALMA chair to President ELLEN JOHNSON SIRLEAF in the side-lines of the AU Summit in Addis Ababa, Ethiopia, ALMA is an alliance of African Heads of State and Government working to end malaria-related deaths.

This body was founded by African Heads of State to utilize their individual and collective power across country and regional borders.

Friday, January 27, 2012

* Mtoto Azra Vuyo Jack aendelea kukulia Mahabusu, wazazi wake watuhumiwa kukutwa na madawa ya kulevya huko Mbeya


Mtoto AZRA VUYO JACK akiwa amelala.


AZRA akiwa amepakatwa na baba yake VUYO JACK nje ya mahabusu ya mahakama kuu ya Mbeya.


Baba na Mama AZRA wakiwa na mtoto wao wakisubiri kuingia Mahakamani.


Msamaria mwema EMILY MWAITUKA ndiye aliyejitolea kumhudumia mtoto AZRA huko mahabusu kwa kumpelekea maziwa kila siku.


Hili ndilo gari la wazazi wa AZRA na ambalo lilitumika kubeba madawa hayo.


AZRA VUYO JACK, Mtoto aliyezaliwa mahabusu na kuendelea kukulia mahabusu.

Wakati Tanzania ikiwa imeridhia mkataba wa kimataifa wa kutekeleza na kulinda haki za watoto na kusimamia kwa karibu ulinzi wa haki za binadamu, sasa serikali ina kila sababu ya kuangalia haki za watoto walioko gerezani kwa makosa ya wazazi wao.

Miongoni mwa haki ambazo serikali inapaswa kuchunguza kwa undani na kubainisha kisa kilichosababisha mtoto mdogo wa kike wa miezi sita , Azra Vuyo Jack, ajikute yeye na wazazi wake wakiwa katika mahabusu ya gereza la Ruanda jijini Mbeya wakikabiliwa na tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya.

Azra ambaye kwa jina la utani, kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Mbeya yetu huko gerezani anaitwa Merryciana au bibi jela jina ambalo limezoeleka zaidi mbali ya jina lake halisi alilopewa na wazazi wake la Azra.

Mtoto huyo wa kike aliendelea kukua katika tumbo la mama yake akiwa gerezani, hatimaye alizaliwa salama Julai 15 mwaka jana katika hospitali ya wazazi meta.

Mama yake ni Anastazia Cloete (27) mwenye asili ya kizungu, raia wa Afrika ya kusini.

Cloete alikamatwa mwaka juzi, Novemba katika mpaka wa Tanzania na Zambia , mji mdogo wa Tunduma akiwa mjamzito na kutupwa mahabusu katika gereza hilo hali iliyomfanya aendelee kulea ujauzito wake.

Uchunguzi wa kina uliendelea kufanywa na madaktari wa hospitali hiyo hadi alipojifungua salama.

Uchunguzi wa tukio la mtoto huyo hadi sasa umezusha mwendelezo wa harakati za kihabari na wanaharakati wa haki za binadamu kuona umuhimu wa kuondolewa kwa mtoto huyo ambaye kwa muda wote tangu azaliwe amekuwa akitumia maziwa ya kopo na hanyonyeshwi na mama yake mzazi.

Mmoja wa ya wasamaria wema aliyejitolea kuwahudumia watuhumiwa hao waliyokumbwa na tuhuma za kukutwa na dawa hizo ni Emily Mwaituka ambaye amekuwa akifanya kazi kubwa ili kuhakikisha mtpto anakuwa na afya nzuri kwa kununuliwa makopo mawili ya maziwa kila wiki tangu alipozaliwa julai, mwaka jana.

Mwaituka anasema amekuwa akinunua kopo moja la maziwa ya unga aina ya SMA 1 ambalo huuzwa sh 26000 na anapaswa kununua makopo mawili ili kuweza kumudu mahitaji ya mtoto huyo wa kike ambaye hanyonyi maziwa ya mama yake mzazi anayesubiri hatima ya kesi inayomkabili akiendelea kuwa mahabusu kwenye gereza la Ruanda jijini Mbeya.

Kumbukumbu za tukio hilo tulizonazo zinaonyesha kuwa raia hao wawili wa Afrika ya Kusini, waliokuwa wakiishi mtaa wa 2A Valley Road – Schaapkraal –Capetown walikamatwa na kilo 42 .5 za dawa za kulevya Novemba 18 mwaka juzi katika mpaka wa Tunduma na kufunguliwa – jalada namba TDM/IR/1763/2010.

Katika tukio hilo ambalo Vuyo na Cloete walinaswa na dawa hizo walizozificha kwenye gari aina ya Nissana Hard body yenye namba za usajili CA – 508 – 656 lililokuwa likimilikiwa na Vuyo Jack waliokuwa wakitokea mkoani Morogoro kuelekea Afrika ya Kusini, Cloete alikuwa akisoma katika chuo cha Capetech.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ambazo zimethibitishwa na Mkemia Mkuu wa Serikali dawa hizo za kulevya ni paketi 26 za cocaine zenye uzito wa kilo 28.5 paketi tatu za Heroine zenye uzito wa kilo 3.25 na paketi nane aina ya Morphine zenye uzito wa kilo 3.25, madawa hayo yote yanathamani ya zaidi ya sh bilioni 1.2.

Wednesday, January 25, 2012

* Rais Jakaya Kikwete amewasili mjini Davos nchini Uswisi kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa kimataifa wa uchumi wa Dunia, WEF


President JAKAYA KIKWETE is received by the Minister for Agriculture, Food Security and Cooperatives Professor JUMANNE MAGHEMBE as he arrives at the Davos Sheraton ahead of the four day World Economic Forum held annually in the mountainous health resort.

The forum, that goes under the theme: " The Great Transformation: Shaping New Models", is being attended by among others President KIKWETE is also scheduled to hold a number of private meetings and bilateral talks with prominent world leaders and entrepreneurs, besides attending interactive sessions on different issues.


President JAKAYA KIKWETE holding a preparatory meeting with his delegations soon after arrival at the Davos Sheraton ahead of the start of the four day World Economic Forum held annually in the mountainous health resort.

Tuesday, January 24, 2012

* Makamu wa Rais Dkt Mohammed Bilal Ziarani Mkoa wa Tanga, akagua ukuta wa kuzuia maji ya Bahari.


Makamu Wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akikata utepe kuzindua rasmi Jengo la Ofisi ya Idara ya Maji, lililopo Wilaya ya Pangani, wakati alipoanza ziara yake ya Mkoa wa Tanga Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, CHIKU GALAWA (kushoto) ni Mkurugenzi wa Maji wa wilaya hiyo, MOHAMMED HAMIS.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED BILAL, akisikiliza maelezo kuhusu ukuta huo unaozuia maji ya Bahari unaobomoka kutokana na mabadiliko ya Tabia nchi na kutishia amani ya wakazi wa maeneo hayo.

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Shein akutana na wizara ya kazi pamoja na Afya kwa nyakati tofauti


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt ALI MOHAMMED SHEIN alipokuwa akizungumza na watendaji wa Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati, Ikulu Mjini Zanzibar katika mpangilio wake wa kuzungumza na kila Wizara ya Serikali ya Zanzibar katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja.



Baadhi ya Watendaji wa Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji naNishati, wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt ALI SHEIN alipokuwa akizungumza na watendaji hao Ikulu Mjini Zanzibar.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt ALI SHEIN alipokuwa akizungumza na watendaji wa Wizara Afya katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar katika mpangilio wake wa kufanya mazungumzo na kila Wizara ya Serikali yake.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt ALI SHEIN akizungumza na watendaji wa Wizara Afya, Ikulu Mjini Zanzibar ukiwa ni mpangilio wake wa kuzungumza na kila Wizara ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Thursday, January 19, 2012

* Rais Jakaya Kikwete na Dakta Mohammed Bilal waomboleza kifo cha mbunge wa Arumeru Mashariki, Jeremiah Sumari

Rais JAKAYA KIKWETE akiweka saini kitabu cha maombolezo.


 Makamu wa Rais Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akiweka saini kitabu maombolezo.



Picha mbili tofauti zikiwaonesha Rais JAKAYA KIKWETE pamoja na Makamu wake Dakta MOHAMMED GHARIB bilal wakitoa Pole kwa familia ya Marehemu JEREMIAH SUMARI aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki ambae amefariki dunia kutokana maradhi ya kisukari.

* H-BABA akamilisha wimbo wa Sina Raha aliomshirikisha Banza Stone

Mwanamuziki H-BABA
MSANII mahiri wa muziki wa kizazi kipya nchini, Hamis RamadhanH-Baba’ amekamilisha kibao chake kipya kinachokwenda kwa jina la Sina Raha, akimshirikisha gwiji wa muziki wa dansi nchini, Ramadhan Masanja, ‘Banza Stone’ Mwalimu  wa Walimu.

Akizungumza na Mtandao wa Sufianimafoto, H-Baba, alisema kuwa kibao hicho ni miongoni mwa nyimbo zake 10 zitakazokamilisha albam yake mpya itakayokwenda kwa jina la ‘Shika hapa acha Hapa’ inayotarajia kuingia sokoni mwezi wa tatu mwaka huu.
Aidha alisema kuwa wimbo ambao amemshirikisha Banza Stone, amerokodia katika Studio ya Allan Mapigo, ambapo tayari amekamilisha maandalizi ya kurekodi video ya wimbo huo mwishoni mwa wiki hii.
H-Baba alisema kuwa katika wimbo huo mashabiki wake watarajie kupata vitu tofauti ikiwa ni pamoja na staili mpya na midundo iliyo ‘shiba’ na sauti murua ya Banza Stone, aliyeonyesha uwezo wake katika wimbo huo.
Alizitaja studio alizorekodia nyimbo zake zitakazokamilisha albam hiyo kuwa ni pamoja na KGC Studio, Maneke Studio na Allan Mapigo, zote za jijini Dar es Saam.
Pia alizitaja baadhi ya nyimbo zitakazokuwamo katika albam hiyo kuwa ni pamoja na, Nipe Kidogo, Shika Kichwa, Kinacho Niumiza, Zaidi yako Wewe na Nimpende Nani.

* Rais Kikwete aongoza mamia katika mazishi ya Regia Mtema,Ifakara



Rais JAKAYA KIKWETE akiwa katika Mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Chadema marehemu REGIA MTEMA.

Wednesday, January 18, 2012

* Ujumbe wa Abort Fund wamtembelea Makamu wa Rais Dakta Mohammed Bilal



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akizungumza na ujumbe kutoka Abort Fund, ANDY WILSON katikati na Dkt AYOUB MAGIMBA, wakati walipomtembelea ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam.

Tuesday, January 17, 2012

* Mwili wa aliyekuwa mbunge wa viti maalum kupitia Chadema Marehemu Regia Mtema waagwa rasmi leo Jijini Dar es Salaam


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL na mkewe Mama ZAKHIA BILAL, wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum kupitia CHADEMA, marehemu REGIA MTEMA, aliyefariki mwishoni mwa wiki kwa ajali ya gari eneo la Daraja la Mto Ruvu ambapo Mwili wa marehemu REGIA umeagwa katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam na kusafirishwa kuelekea nyumbani kwao Ifakara kwa maziko.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL na mkewe Mama ZAKHIA BILAL, wakiagana na wanafamilia ya aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum kupitia CHADEMA, marehemu REGIA MTEMA.



Waziri Mkuu, MIZENGO PINDA na mkewe Mama TUNU PINDA, wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum kupitia CHADEMA, Mwili wa marehemu REGIA umeagwa katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam na kusafirishwa kuelekea nyumbani kwao Ifakara kwa maziko.


Spika wa Bunge ANNE MAKINDA, akitoa wasifu wa marehemu katika shughuli zake za kibunge na Salam za rambirambi kwa niaba ya Bunge.


Askari wa Bunge wakibeba Jeneza kuelekea mahala palipoandaliwa rasmi kwa ajili ya shughuli za kuaga kabla ya mwili wa Marehemu REGIA kusafirishwa kuelekea Ifakara kwa ajili ya Maziko. 

Friday, January 13, 2012

Rais Jakaya Kikwete atembelea eneo la Mabwepande na kupokea Seti ya Vyombo pamoja na taa zinazotumia nguvu ya Jua



Rais JAKAYA KIKWETE na mama SALMA KIKWETE wakioneshwa maeneo ya makazi mapya ya walioathirika na mafuriko katika bonde la Msimbazi walipotembelea eneo hilo.


Rais JAKAYA KIKWETE akipokea seti ya vyombo vya nyumbani na taa inayotumia nguvu za jua kutoka kwa Mkurugenzi wa Home Shopping Centre GHARIB SAID MOHAMMED ambaye kampuni yake imejitolea kugawa seti kama hizo pamoja na taa kwa kila familia 655 zilizohamishiwa Mabwepande baada ya kuathirika na Mafuriko katika bonge la Msimbazi, GHARIB pia ameahidi kujenga shule ya msingi ya eneo hilo pamoja na kituo cha polisi.

* Rais Jakaya Kikwete na Mkewe mama Salma wameiaga miili ya wanajeshi wawili waliofariki Dunia hivi karibuni Jijini Dar es Salaam


Rais JAKAYA KIKWETE na mkewe mama SALMA KIKWETE wakitoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Kamishna wa Magereza ELIAS MTIGE NKUKU,aliyefariki juzi kabla ya kusafirishwa kwenda kwao mkoani Singida, Shughuli ya kumuaga imefanyika katika bwalo la jeshi la Magereza Ukonga jijini Dar es salaam.


Rais JAKAYA KIKWETE na mkewe mama SALMA KIKWETE wakitoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Kanali PASTORY KAMUGISHA wa JWTZ aliyefariki juzi kabla ya kusafirishwa kwenda kwao mkoani Kagera, Shughuli ya kumuaga marehemu imefanyika katika kambi ya jeshi ya Lugalo Jijini Dar es salaam.

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Shein ahudhuria tamasha la Taarabu rasmi katika ukumbi wa Salama Bwawani mjini Unguja


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt ALI MOHAMMED SHEIN akiangalia taarab Rasmi iliyocharazwa na Kikundi Culture Musical Club ndani ya Ukumbi wa Salama Bwawani katika kusheherekea Miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar,wa kwanza kulia ni Mama Balozi SEIF ALI IDDI Mkuu wa Mkoa wa Mjini Mahgaribi ABDALLAH MWINYI KHAMIS na kushoto ni Waziri wa habari Utamaduni na Michezo ABDILLAH JIHAD HASSAN.


Mwimbaji FATMA ISSA wa Kikundi cha Culture Musical Club akiwaburudisha mashabiki katika ukumbi wa Salama Bwawani kwa nyimbo ya"Umewashika" katika sherehe za Kutimiza miaka 48 ya Mapinduzi ya
Zanzibar.


Wasanii wa kikundi cha muziki cha Culture Musical Club wakicharaza ala katika hafla maalum ya kusheherekea miaka 48 yaMapinduzi Zanzibar katika ukumbi wa Salama Bwawani.

Thursday, January 12, 2012

* Kamati kuu ya CCM Taifa yamchagua Mohammed Raza kuwania nafasi ya Uwakilishi wa Jimbo la Uzini, wilaya ya kati Unguja

Mohammed Raza, Kada wa Siku nyingi wa chama cha Mapinduzi CCM




Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt JAKAYA MRISHO KIKWETE (katikati) akiendesha kikao cha Kamati Kuu ya CCM Taifa, katika ukumbi wa chama hicho Kisiwandui Mjini Zanzibar.

* Maadhimisho ya miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar yafanyika Visiwani humo


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt ALI MOHAMMED SHEIN akizungumza na wananchi wa Zanzibar katika kilele cha miaka 48 ya mapinduzi matukufu ya Visiwa hivyo.


Rais wa Zanzibar  Dkt ALI MOHAMMED SHEIN akikagua gwaride la vikosi vya ulinzi wakati wa Sherehe za kutimia kwa miaka 48 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amaan.







Askari wa Kikosi cha JWTZ wenda kwa miguu kikipita mbele Rais wa Zanzibar Dkt ALI MOHAMMED SHEIN na kutoa heshima kwa mwendo wa kurukaruka wakati wa sherehe za Kilele cha kutimia Miaka 48 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar


Askari wa Kikosi cha Polisi FFU kikipita mbele kwa kutoa heshima ya gwaride mwendo wa pole katika kilele cha miaka 48 ya Mapinduzi Zanzibar zilizofanyika jana katika uwanja wa Amaan Mjini Zanzibar.




Wananchi waliohudhuria katika sherehe za kutimia miaka 48 ya mapinduzi ya Zanzibar wakifuatilia kwa makini harakati za sherehe zinavyoendelea katika uwanja wa amaan Mjini Zanzibar.


Wananchi wakishuhudia mizinga 21 ikipigwa