Friday, January 13, 2012

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Shein ahudhuria tamasha la Taarabu rasmi katika ukumbi wa Salama Bwawani mjini Unguja


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt ALI MOHAMMED SHEIN akiangalia taarab Rasmi iliyocharazwa na Kikundi Culture Musical Club ndani ya Ukumbi wa Salama Bwawani katika kusheherekea Miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar,wa kwanza kulia ni Mama Balozi SEIF ALI IDDI Mkuu wa Mkoa wa Mjini Mahgaribi ABDALLAH MWINYI KHAMIS na kushoto ni Waziri wa habari Utamaduni na Michezo ABDILLAH JIHAD HASSAN.


Mwimbaji FATMA ISSA wa Kikundi cha Culture Musical Club akiwaburudisha mashabiki katika ukumbi wa Salama Bwawani kwa nyimbo ya"Umewashika" katika sherehe za Kutimiza miaka 48 ya Mapinduzi ya
Zanzibar.


Wasanii wa kikundi cha muziki cha Culture Musical Club wakicharaza ala katika hafla maalum ya kusheherekea miaka 48 yaMapinduzi Zanzibar katika ukumbi wa Salama Bwawani.

No comments:

Post a Comment