Tuesday, May 29, 2012

* Media Briefing note for the Global 2013 Smart Partnership Dialogue to be held in DAR ES SALAAM, TANZANIA – 24TH TO 28TH MAY, 2013



Tanzania will host the next Smart Partnership Dialogue that is scheduled to take place from 24th to 28th May, 2013 in Dar es Salaam. President Jakaya Mrisho Kikwete, is expected to officiate the National launch at noon today Tuesday May 29, 2012 at the Karimjee Hall grounds in Dar es salaam. President Kikwete had agreed to host the event during the last dialogue that took place in Putrajaya, Malaysia in June, 2011 - branded the Langkawi International Dialogue.

The Smart Partnership Dialogues are a brainchild of the Commonwealth Partnership for Technology Management. The CPTM which is the social and scientific interlinkage arm of the Commonwealth, has since 1995 undertaken in collaboration with willing national partners to provide a forum that cuts across the east-west, have, have not’s and the developed and developing dichotomy for the discussion of topical subjects in a conducive inclusive, open dialogue. Inspired by the increasing need to ensure a win-win interrelationship between actors, the CPTM, in collaboration with the host country undertake to provide an ambient setting where individuals from all walks of life and professions can meet and hold serious discourse on selected subjects every two years.

To ensure that these dialogues are successful, a two pronged approach is utilized. The first is when the host country convenes a National Dialogue. This involves the gathering together of different sectors of the host community and coming up with a topical issue that is not just locally relevant, but which resonates internationally and merits a grander discourse and focus. The second is when the Host country in collaboration with the CPTM plan for, invite participants and hold an international open dialogue on the selected topic, in essence, host a SMART DIALOGUE. As hosts, the kicking off of the National Dialogue is very crucial.

It is a means for creating National and International awareness of the next host of the Dialogue and avails the opportunity to announce the dialogue venue, topic and dates. The Launch of the National Campaign for the Dialogue in Tanzania will take place on the 29th May, 2012 at the Karimjee Hall Grounds from 10:00 am to 11:00 am. The Host and Patron Advisor for the 2013 |Smart Partnership Dialogue, H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania will officially launch preparations for the 2013 Dialogue and introduce the Theme for the Dialogue (Leveraging Technology for Africa’s Socio-Economic Transformation) announce the date for the Dialogue (24th to 28th May, 2013) and the venue (Dar es Salaam) issue a holistic invitation to both the citizens of Tanzania as well as the International Community at large, and share his vision for the Dialogue.

The Dialogue has been branded the GLOBAL 2013 SMART PARTNERSHIP DIALOGUE in anticipation of interest the chosen theme is likely to raise. Technology is a global phenomenon, a global concern, a global topical issue. It is therefore more than likely that a Dialogue on Technology for development shall merit global attention and have a global audience/participation. The Execution of the preparation will be undertaken under the guidance of the Chief Secretary who is the Convener of the Dialogue.

The Chief Secretary will be supported by a National Steering Committee that comprises of Permanent Secretaries from All Ministries as well as Representatives of Keyline Sectors both on Mainland Tanzania and Zanzibar. A Focal Point Team from the Ministry of Foreign Affairs will spearhead the logistical and liaising activities necessary for the successful execution of the Dialogue. The Team will over time incorporate Members from different Links A Resource Group with an Advisory role comprising of key members of the Academia, Business and Corporate Community, Youth, Labour, Culture, Industry and Media has been set up under the leadership of Professor Samuel Wangwe.

Following the National Launch, the next step is scheduled to be contact with different Links within Tanzania who will in turn be linked with counterparts interested in participating in the Dialogue in 2013. A National Dialogue to discuss the theme will follow thereafter. Other African countries that have hosted the Smart Partnership Dialogues include Botswana, Namibia, Zambia, Zimbabwe, Mozambique, Swaziland, Lesotho and Uganda that has hosted it twice. Other countries include Barbados, and Malaysis that has hosted the dialogue nine times.

 Issued by

THE FOCAL POINT TEAM, GLOBAL 2013 SMART PARTNERSHIP DIALOGUE, MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION

Sunday, May 27, 2012

* Vurugu Zanzibar,,Hali imeanza kuwa shwari



Hali ilivyokuwa leo Asubuhi katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar



Kiongozi wa Jumuiya ya kikundi cha uamsho, Sheikh FARID HADI AHMED


Maelfu wa Wazanzibari wakiongozwa na Taasisi za Kiislamu na Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar JUMIKI, wakifanya matembezi ya amani katika barabara za Zanzibar na kupeleka ujumbe wao kwa viongozi wa Serikali ya Zanzibar na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Umoja wa Mataifa wakitaka Zanzibar huru, ambapo baadhi ya watembeaji hao wakiongozwa na Kiongozi wa Jumuiya hiyo, Sheikh FARID HADI AHMED na viongozi wengine.

Na ; Mwandishi wetu 

Waandamanaji hao wakiongozwa na Sheikh Farid Hadi Ahmed walitembea kutoka viwanja vya Lumumba na kupitia barabara ya Kinazini, Mpigaduri, Michenzani Maskani ya CCM Kisonge, kwa Biziredi na kurudi tena viwanja vya Lumumba.

Maandamano walioyaita matembezi ya amani yalifanyika na kuhudhuriwa na maelfu ya wazanzibari ambapo awali kuliandaliwa kongamano kubwa lililoandaliwa na Taasisi za Kiislamu kwa kushirikiana na Jumuiya ya Uamsho JUMIKI kwa lengo la kuzungumzia mfumo wa elimu Zanzibar.

Akizungumza na maelfu ya wazanzibari kabla ya kuanza maandamano hayo yaliitwa ni matembezi ya amani, Sheikh Farid alisema wazanzibari wana haki kama walivyokuwa na haki wananchi wengine ulimwenguni kote kudai haki yao ndani ya nchi yao. “Sisi wazanzibari kama wananchi wengine wowote duniani tuna haki ya kikatiba kudai nchi yetu kama walivyodai Sudan ya Kusini, mbona Sudan ya wameweza kujitenda na kupata nchi yao kwa nini sisi kama wazanzibari tusikubaliwe kudai nchi yetu sasa sisi tunampelekea salam katibu mkuu wa umoja wa mataifa kumwambia kuwa wazanzibari sasa wanataka nchi yao” alisisitiza Sheikh Farid huku akiungwa mkono na wananchi hao.

Awali Sheikh Farid alisema salamu hizo anataka zimfikie Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Kin moon ambaye kwamba wazanzibari wamechoshwa na kuwepo ndani ya Muungano ambao umedumu kwa miaka 48 lakini bado ukiwa na kero nyingi na malalamiko ambayo yanaonekana utatuzi wake ni mdogo na usiowezekana ambapo alisema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hauna manufaa yena na wazanzibari.

Katika kuonesha kwamba hawataki tume ya katiba ije kuchukua ya maoni ya katiba mpya Sheikh Farid alisema wanataka kwanza kuamuliwe suala la Muungano kabla ya jambo lolote na kuahidi kwamba wataendelea kufanya makongamano, mihadhara na maandamano kwa kadiri wawezavyo hadi hapo Serikali itakaposikia kilio hicho. “Ujumbe huu tunautoa kwa Ban Kin moon, na kwa ulimwengu mzima lakini pia tunataka rais wetu Dk Shein asikie kilio hiki na Rais Kikwete ambaye yeye ni mtetezi wa haki za binaadamu na pia ni mfuatiliaji wa nchi zinazovunja haki za binaadamu tunataka asikie kilio cha wazanzibari kuwa wanataka nchi yao” alisema.

Alisema juzi wamefanya maombi maalumu ya kumuombea Rais wa Zanzibar lengo likiwa ni kumjaaliwa kheri na awe na maamuzi sahihi juu ya wananchi wa Zanzibar sambamba na kuwaomba Makamu wa Kwanza na makamu wa Pili wa Zanzibar kusikia kilio cha wazanzibari wasiotaka Muungano. “Tunamuomba Rais wetu Dk Shein, Makamu wa Kwanza Maalim Seif na Makamu wa Pili Balozi Seif kwamba sisi wazanzibari tunahitaji Zanzibar huru, tunahitaji heshima ya nchi yetu na tupo tayari kwa lolote kwa hivyo tunataka salamu hizi na ujumbe huu ukufikieni” alisema Sheikh Farid huku akiungwa mkono na maelfu waliohudhuria katika kongamano hilo ambalo awali liliandaliwa kwa lengo la kuzungumzia masuala la elimu na mfumo wake.

Waandamanaji hao walianza kutembea kwa utaratibu maalumu huku magari yakisimama na kuwapisha bila ya kuwepo jeshi la polisi ambapo viongozi wa jumuiya hiyo na wananchi wengine waliongoza utaratibu huo na kutembea katika barabara kwa utaratibu mzuri hadi kumaliza maandamano yao waliyoyaita matembezi ya amani.

Baadae jeshi la polisi lilifika katika eneo ambalo kumefanyika maandamano hayo na kufungua mabango yao ya kuwataka watu kuondoka lakini wakati magari hayo ya polisi matatu yanafika eneo hilo la Kariakoo tayari ummati mkubwa ulikuwa umeshapita katika eneo hilo na hivyo kuingia ndani ya magari yao na kuondoka kwa salama.

Awali akitoa mada katika kongamano hilo, Maalim Abdulhafidh Malelemba alisema sekta ya elimu imekuwa ikidorora Zanzibar kutokana na kukandamizwa na mambo ya Muungano ambapo kila mwaka wanafunzi wanapofanya mitihani hufelishwa kwa makusudi huku idadi ya wanafunzi wanaokwenda katika vyuo vikuu wakiwa kidogo kutokana na kufelishwa katika mitihani ambapo husainiwa na baraza la mithani Tanzania NECTA.

Wakizungumza katika nyakati tofauti katika kongamano hilo, baadhi ya walimu walisema kukosekana kwa baraza la mitihani Zanzibar kusimamia mitihani ya elimu ya juu ndio sababu ya wazanzibari kufelishwa kwa wingi na kushindwa kuingia katika vyuo vikuu kwa kuwa wanafunzi wengi wa Zanzibar hufelishwa.

Walimu hao walitoa ushahidi wa hivi karibuni wa kufelishwa wanafunzi wa kidatu cha nne ambapo walisema lile ni tukio la makusudi lililofanywa na baraza la mitihani ikiwa ni kuwadhoofishwa wanafunzi wa Zanzibar ili wasiendelee katika masomo kwa kuwafelisha.

Thursday, May 24, 2012

* Dakta Bilal ahudhuria Mkutano wa Wakuu wa nchi Kuhusu maendeleo Barani Afrika



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akihutubia kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Maendeleo Endelevu katika Bara la Afrika mjini Gaborone.
 
 
 Na ; Mwandishi Wetu
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Dkt Mohammed Gharib Bilal amemwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika mkutano wa Maendeleo Endelevu Afrika unaolenga katika kujumuisha thamani ya Rasilimali Asilia katika kupima maendeleo ya kiuchumi katika nchi za Afrika.
Katika mkutano huo, Tanzania imeunga mkono kuanzishwa kwa mfumo wa kujumuisha thamani ya raslimali asilia ambao utahusishwa kwenye tathmini ya pato la taifa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na  vijavyo.
Makamu wa Rais Akihutubia mkutano huo amesema, mchango wa rasilimali asilia zina nafasi kubwa katika kuchangia katika pato la taifa lakini ili mchango wake utambulike, nchi zinahitajika kuwa na utaratibu wa kuzifanyia tathmini hasa kuhusu matumizi yake na faida zake katika uchumi huku pia athari zake zikitazamwa hasa zile zinazotokana na kupoteza uhalisia wa mazingira ama kuharibu mazingira ya nchi.
Kwa mujibu wa Makamu wa Rais, dhana ya kutathmini mazingira na kujumisha raslimali asilia kwenye hesabu za pato la taifa, kunaweza kusaidia nchi kufikia maamuzi ambayo yataliwezesha taifa kupata maendeleo endelevu hali ambayo itachangia jitihada za kupunguza umaskini na kukuza uchumi.
Dkt. Bilal ameueleza mkutano huo kuwa, Tanzania iliona umuhimu wa raslimali asilia tangu nchi ilipopata uhuru mwaka 1961 ambapo iliweza kutenga asilimia 30 ya eneo la nchi kwa ajili ya wanyama na viumbe hai, Tena ziliwekwa sera nzuri zilizolinda uvunaji wa raslimali hizo kwa manufaa ya taifa.
Makamu wa Rais ameueleza mkutano huo pia kuwa, nchi nyingi za Afrika zinategemea kilimo kama njia kuu ya uchumi na sekta hii bado inategemea mvua huku ikihusisha wakulima wadogo wadogo hali ambayo inaonesha ma mazingira yataharibiwa ni wazi maisha ya wengi yataathirika.
Anasisitiza kuhusu kuwepo kwa mfumo mpya wa kilimo unazingatia kutoharibu rasilimali asilia na wakati huo huo kuhakikisha kuwa mazingira yanabaki kama yalivyo ili yasaidie jamii zijazo.
Katika mkutano huo, Tanzania na Botswana zimepongezwa kwa uhifadhi wa maliasili na mazingira kwa ajili ya kizazi cha sasa na cha baadaye.
Mkutano huo wa pia unahudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka nchi zipatazo 11 wakiwemo Marais Hifikupenye Pohamba wa Namibia, na Bibi Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia.
                                                        = = = =

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akizungumza na Rais wa Liberia Bibi ELLEN JOHNSON SIRLEAF kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Maendeleo Endelevu Barani Afrika unaofanyika mjini Gaborone.
 
 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Nchi pamoja na wawakilishi  kutoka nchi za Afrika waliohudhuria mkutano wa Maendeleo Endelevu katika Bara la Afrika.

Wednesday, May 23, 2012

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Shein akutana na Uongozi wa Wizara ya Fedha


Rais wa Zanzibar Dakta Ali Mohammed Shein Akizungumza na Viongozi wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais - Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo ukiwa ni mpango kazi wa Ofisi hiyo.

* Msondo Ngoma kupagawisha wapenzi wake Ndani ya Masasi


Rajabu Mhamila - Msemaji wa Bendi ya Msondo


Baadhi ya Wanamuziki wa Bendi ya Msondo Ngoma

Na : Mwandishi wetu

BENDI Kongwe ya Msondo ngoma ya jijini Dar es salaam inatarajia kufanya uzinduzi wa ukumbi mpya kabisa wa kisasa wa burudani  wa Emirate Hall uliopo Masasi June 2 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari Msemaji wa bendi hiyo Rajabu Mhamila 'Super D' Alisema wamealikwa kwa ajili ya kutoa burudani siku ya ufunguzi wa ukumbi huo ambapo watatoa burudani isiyo na kifani

"Unajua sisi ni baba ya Muziki nchini ndio mana wapenzi wengi wanaitaji burudani kutoka kwetu ndio mana tunapopata nafasi ya kwenda mikoani tunakwenda kama hivi tumealikwa kutoa burudani siku hiyo tutatoa burudani ya uwakika" alisema

Siku hiyo tutapiga vibao vetu vya zamani na vipya kwa sasa alivitaja baadhi ya vibao vitakavyonogesha uzinduzi huo kuwa ni Suluhu wa Shabani Dede, Nadhiri ya Mapenzi wa Juma Katundu na Baba Kibene wa Eddo Sanga hizo ni baadhi ya nyimbo mpya zitakazonogesha siku hiyo vile vile watapiga nyimbo zao za zamani zilizotamba wakati huo.

Alisema Super D Kundi hilo litaambatana na wanamziki wake wote wakiwemo wakongwe katika mziki wa Dansi Nchini Maalimu Gulumo ' Kamana' Saidi Mabela ' DKT Mabela' na wengine wote watafanya vitu vyao siku hiyo kwa ajili ya kukonga nyoyo za mashabiki wao wa Masasi Aliongeza Super D. 

* Mama Asha Bilal Mgeni Rasmi maadhimisho ya miaka miwili ya Taasisi ya Tushikamane


Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama ASHA BILAL, akisoma hotuba yake wakati wa hafla ya maadhimisho ya kusherehekea kutimiza miaka miwili ya Taasisi ya Tushikamane Pamoja Foundation, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee.



Mchezaji wa mpira wa Kikapu HASHEEM THABEET, akipita jukwaani na vazi la asili kwa mikogo  wakati wa hafla ya maadhimisho ya kusherehekea kutimiza miaka miwili ya Taasisi ya Tushikamane Pamoja Foundation.


Mke wa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mama MARGARETH SITTA, akipita jukwaani na vazi la asili kwa mikogo, wakati wa hafla ya maadhimisho ya kusherehekea kutimiza miaka miwili ya Taasisi ya Tushikamane Pamoja Foundation iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Thursday, May 17, 2012

* Mafisango sasa kuagwa TCC Chang'ombe,Badala ya Viwanja vya Leaders


Marehemu PATRICK MAFISANGO


Mwili wa kiungo mahiri wa Simba Sports Club Patrick Mafisango (32), sasa utaagwa kwenye Uwanja wa TCC club, Chang'ombe, Dar es Salaam, kuanzia saa 3:00 asubuhi badala ya Leaders Club, Kinondoni, kama ilivyotangazwa hapo awali.

Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Geoffrey Nyange amesema kwamba wamehamishia shughuli ya kuuga mwili huo Uwanja wa Siga ratiba nyingine zote zinabaki kama ilivyotangazwa awali.

Mafisango amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika eneo la Keko jirani na Chuo cha VETA jijini Dar es Salaam.

Mafisango alifariki kutokana na ajali iliyotokea wakati gari alilokuwa akiendesha lilipogonga mti ulio pembezoni mwa barabara ya Chang’ombe majira ya saa kumi kasorobo alfajiri ambapo Marehemu alifariki papo hapo.

Kwenye gari aliyokuwamo Mafisango, kulikuwapo na abiria wengine wanne lakini ni Mafisango pekee ndiye aliyefariki dunia.

Mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili tayari kwa kusafirishwa kwenda kwao Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ambako atazikwa.

Ingawa alikuwa na uraia wa Rwanda na akiichezea timu ya taifa ya nchi hiyo Amavubi, Mafisango alikuwa ni mzaliwa na raia wa DRC na uamuzi wa kuzikiwa huko ni wa familia yake.

Msiba wa Mafisango uko katika eneo la Keko Toroli jirani na kituo cha Chang’ombe Maduka Mawili (Njia Panda Sigara).

Mwili wa marehemu unatarajiwa kuagwa kesho Ijumaa saa nne asubuhi katika viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar es Salaam kabla ya mwili wake kusafirishwa kwenda Kinshasa majira ya saa kumi jioni.

Mafisango alizaliwa Machi 30, 1980 huko Kinshasa Zaire wakati huo, na ameacha mke na mtoto mmoja wa kiume,anayeitwa Chris Paul, mwenye umri wa miaka mitano.

Mafisango ameichezea Simba kwa msimu mmoja tu akitokea Azam ya Dar es Salaam lakini kabla ya hapo alichezea pia TP Mazembe ya DRC, APR ya Rwanda na pia aliwahi kuwa nahodha wa Amavubi kwa takribani miaka mitano.

Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, Makamu wake, Geofrey Nyange na wajumbe wa kamati ya watendaji wameeleza kusikitishwa kwao na msiba huo mkubwa kwa klabu na wamewataka wana Simba wote kuwa watulivu na kumwombea marehemu Mungu amlaze mahali pema peponi.

Uongozi wa Simba umeahidi kwamba utatoa taarifa nyingine zozote muhimu kwa wananchi ili wafahamu kuhusu msiba huo pale itakapotokea.



* Profesa Tibaijuka, Dakta Huvisa wapewa meno kuanza zoezi la Bomoa Bomoa Nyumba zilizojengwa maeneo ya ufukweni


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL amekutana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa ANNA TIBAIJUKA na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Bi TEREZYA HUVISA, kwa mazungumzo na kupokea taarifa ya zoezi la bomoa bomoa ya nyumba zilizojengwa maeneo ua Ufukweni, ambalo linatarajia kuanza hivi karibuni,Mazungumzo hayo yamefanyika Ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu Dar es Salaam.

Katika picha kutoka (kushoto) ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka (kulia) ni Mkurugenzi wa Mazingira, Dkt, Julius Ningu na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt, Terezya Huvisa.

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Shein akutana na Viongozi wa wizara mbalimbali


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk ALI MOHAMMED akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Katiba na Sheria, kuhusu utekelezaji wa mpango kazi wa Wizara hiyo huko Ikulu Mjini Zanzibar.


Viongozi wa wizara ya Viwanda,Biashara na Masoko wakimsikiliza Rais wa Zanzibar Dakta ALI MOHAMMED SHEIN

Sunday, May 13, 2012

Msanii wa Filamu za Kitanzania Juma Kilowoko"Sajuki" amepelekwa nchini India kwa Ajili ya Matibabu

Mwana-Filamu JUMA KILOWOKO "Sajuki" akiwa katika picha mbili tofauti, kulia ni mkewe WASTARA JUMA

Mwana-Filamu Mahiri hapa nchini JUMA KILOWOLO anayejulikana kama SAJUKI katika tasnia uigizaji,amepelekwa INDIA kwa ajili ya kufanyiwa Oparesheni ya kuondolewa uvimbe tumboni, ambapo kwa mujibu wa madaktari nchini humo wanadai kwamba upo karibu na INI.
SAJUKI ameondoka leo katika uwanja wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere akiambatana na mkewe WASTARA JUMA ambae pia ni Mwana-Filamu, hii ni mara ya Pili kupelekwa nchini INDIA ambapo awali alienda kwa lengo la kufanyiwa vipimo vya damu.
Kuondoka kwa SAJUKI kunafuatia Juhudi mbalimbali zilizofanywa na wasanii wa filamu pamoja wadau wengine wa tasnia hiyo wakiwemo viongozi wa juu wa Serikali.
Dua za Watanzania Bado zinahitajika kumuombea kwa mwenyezi mungu Mwana-Filamu SAJUKI ili aweze kutibiwa na kupona na hatimae arejee nchini kuendelea na majukumu yake ya Ujenzi wa Taifa……Ameein.
                                                            
                                               

Mwana - Habari Rachel Mwiligwa kuagwa katika kanisa la ANGLIKANA Ubungo


Marehemu RACHEL MWILIGWA

TANGAZO LA MSIBA
Mwili wa marehemu  RACHEL MWILIGWA aliyekuwa mhariri wa gazeti la MTANZANIA  linalomilikiwa na kampuni ya NEW HABARI CORPOROTAION  utaagwa   tarehe  14.5.2012  katika kanisa la ANGLIKANA UBUNGO jirani na Shule ya msingi ya  national housing.
Waaandishi wahabari  na wadau  wa michezo nchini wanaombwa  kujitokeza kwa wingi kuhudhuria ibada hiyo ambapo baadae saa sita mwili utapelekwa  eneo la GOBA nje  kidogo ya jiji la DSM kwa ajili ya mazishi.
Tunashukuru kwa ushirikiano ulionyeshwa   kutoka waandishi wenyewe,wananchi na wadau wa michezo nchini katika kufanikisha jambo hili.
Taarifa hii ni kwa kujubu wa kaka wa marehemu ALEX CHIMELA
Bwana ametoa  na bwana ametwaa jina la bwana libarikiwe.