Wednesday, May 23, 2012

* Msondo Ngoma kupagawisha wapenzi wake Ndani ya Masasi


Rajabu Mhamila - Msemaji wa Bendi ya Msondo


Baadhi ya Wanamuziki wa Bendi ya Msondo Ngoma

Na : Mwandishi wetu

BENDI Kongwe ya Msondo ngoma ya jijini Dar es salaam inatarajia kufanya uzinduzi wa ukumbi mpya kabisa wa kisasa wa burudani  wa Emirate Hall uliopo Masasi June 2 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari Msemaji wa bendi hiyo Rajabu Mhamila 'Super D' Alisema wamealikwa kwa ajili ya kutoa burudani siku ya ufunguzi wa ukumbi huo ambapo watatoa burudani isiyo na kifani

"Unajua sisi ni baba ya Muziki nchini ndio mana wapenzi wengi wanaitaji burudani kutoka kwetu ndio mana tunapopata nafasi ya kwenda mikoani tunakwenda kama hivi tumealikwa kutoa burudani siku hiyo tutatoa burudani ya uwakika" alisema

Siku hiyo tutapiga vibao vetu vya zamani na vipya kwa sasa alivitaja baadhi ya vibao vitakavyonogesha uzinduzi huo kuwa ni Suluhu wa Shabani Dede, Nadhiri ya Mapenzi wa Juma Katundu na Baba Kibene wa Eddo Sanga hizo ni baadhi ya nyimbo mpya zitakazonogesha siku hiyo vile vile watapiga nyimbo zao za zamani zilizotamba wakati huo.

Alisema Super D Kundi hilo litaambatana na wanamziki wake wote wakiwemo wakongwe katika mziki wa Dansi Nchini Maalimu Gulumo ' Kamana' Saidi Mabela ' DKT Mabela' na wengine wote watafanya vitu vyao siku hiyo kwa ajili ya kukonga nyoyo za mashabiki wao wa Masasi Aliongeza Super D. 

No comments:

Post a Comment