Tuesday, April 10, 2012

* Mwana-Filamu STEVEN KANUMBA azikwa Makaburi ya Kinondoni,mamia Wapoteza fahamu wakati wa Kuuaga Mwili wake


Watoto waliowahi kuigiza na marehemu STEVEN KANUMBA na ambao aliibua vipaji vyao yeye mwenyewe wakiwa wamebea picha ya KANUMBA.

Mama wa Marehemu STEVEN KANUMBA akiweka shada la maua katika kaburi la mtoto wake.



Waombolezaji wa msiba wa Marehemu STEVEN CHARLES KANUMBA wakishusha jeneza lenye mwili wa marehemu kwenye kaburi, tayari kwa kumpumuzisha katika nyumba ya milele kwenye makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.

KANUMBA atakumbukwa kwa kazi yake nzuri katika tasnia ya filamu hapa nchini, ambapo alijitangaza na kuitangaza nchi vyema ndani ya Tanzania na nje ya Tanzania kupitia filamu zake nyingi alizoigiza.



Hali ilikuwa ni ya majonzi na waombolezaji wengi walidondoka chini na kupoteza fahamu kutokana na simanzi.



Gari lililobeba mwili wa marehemu KANUMBA linaondoka katika viwanja vya Leaders kwenda Makaburi ya Kinondoni huku likiwa limezungukwa na waombolezaji.

(MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI AMEN)

No comments:

Post a Comment