Thursday, April 26, 2012

* Mabondia Japhet Kaseba na Francis Cheka kupambana siku ya Saba saba

Bingwa Mchezo wa Kickboxing hapa nchini JAPHET KASEBA akisaini mkataba wa kupambana na FRANCIS CHEKA.


Bondia FRANCIS CHEKA akisaini mkataba wa kupambana na JAPHET KASEBA.


Na Mwandishi wetu

Bingwa wa dunia wa ndondi mkanda unaomilikiwa na IBC, Francis Cheka wa Morogoro  amesaini mkataba wa kupigana na  bingwa wa kick Boxing Japhet  Kaseba   katika uzani wa KG 75 utakaofanyika siku ya sabasaba jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kusaini mkataba huo Cheka amesema anashukuru kupata mpambano huo na atahakikisha anaonesha uwezo wake wote katika mchezo huo kwani yeye ni bingwa wa mchezo wa masumbwi na mabondia wengi wanataka kupigana nae.



Mbali na mpambano huo pia kutakua na mapambano ya utangulizi na burudani mbalimbali ambazo mtatangaziwa baadae.
"Najua mabondia wa hapa bongo kila mtu anataka kucheza na mimi tu wanajua mimi ndio nalipa kwa soko la bongo na nitahakikisha kila anaekuja mbele yangu namtandika kifupi Tanzania akuna bondia mwenye uwezo zaidi yangu" alisema Cheka.

"Kaseba nilimpiga kwa K.O tareha 3 October 2009 nilimpinga anataka tena wembe kwa ngua ngumi ni sehemu ya maisha yangu siwezi kukataa na mimi ndio napata ridhiki yangu humu hivyo nitahakikisha anaekuja mbele yangu namtwanga tu bila huruma nitaanza na Mada Maugo 28 April na huyo namuweka kama kiporo".

Promota wa mpambano huo Kaike Siraju amesema mpambano huo utakaofanyika Dar es salaam siku ya sabasaba utakuwa ni mpambano ambao haujawahi kutokea kwa kuwa mabondia hao wanakubalika na mashabiki wa ndani na nje ya Nchi
.

No comments:

Post a Comment