Thursday, April 19, 2012

* Mambo safi Group yaweka kambi kwa ajili ya makamuzi ya MAY DAY


Mkurugenzi wa SF GROOUP OF COMPANIES LIMITED, SELINA KOKA kushoto akimkabidhi gita kiongozi wa kundi la Mambo safi, FABBIAN SALVATORY 'Super Phabby' kwa ajili ya kuweka kambi ya siku saba ili waanze kutoa burudan kwa wakazi wa jiji ifikapo mei mosi mwaka huu.


Mkurugenzi wa SF GROOUP OF COMPANIES LIMITED, SELINA KOKA kushoto akiwa pamoja na kundi la Mambo Safi.

Na Mwandishi Wetu
KUNDI la muziki wa asili na dansi la Mambo Safi  limeanza kambi rasmi leo katika ukumbi wa Harbous Klab kwa ajili ya kujiandaa na sherehe za Mei mosi zitakazofanyika katika ukumbi wa Urafiki Club, Dar es Salaam.

Kundi hilo ambalo sambamba na kutoa burudani hiyo pia linajihusisha na kucheza sarakasi pamoja na Ngonjera litakaa kambi hiyo kwa muda wa wiki moja ili kuweza kujiimarisha.

Akizungumza Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa SF group Camponies ltd ambayo ndio inasinamia kundi hilo Selina Koka alisema katika kambi hiyo watakuwa wakifanya mazoezi katika burudani zote wanazozitoa.

"kundi hili huwa linatoa burudani katika shughuli mbalimbali za kiserikali na hii ni moja ya shughuli za kiserikali na ndio maana tumeamua kuweza kambi ili kuweza kujiandaa vya kutosha kwa ajili ya kusheherekea siku hiyo," alisema.

Aliongeza kuwa kundi hilo ambalo linajumla ya wanamuziki 22 linatarajia kuanza kutoa burudani kwa kila wiki katika ukumbi tofauti kama zilivyobendi nyingine ili kuweza kutoa burudani zaidi.

Naye Mkurugenzi mtendaji wa kundi hilo Phabbian Salvatory 'Super Phabby' alisema wanaliandaa kundi hilo kutoa upinzani kwa bendi nyingine kongwe kama Extra bongo, Twanga na nyinginezo ili kuweza kujiweka katika ramani nzuri ya muziki wa dansi hapa nchini.

"hatutaki kuishia hapa tunataka kuwa kama bendi nyingine na hata tuwashinde kwa kuwapa upinzani mkubwa ili kuweza kuwaonyesha uwezo wetu tulionao," alisema.

No comments:

Post a Comment