Thursday, May 17, 2012

* Profesa Tibaijuka, Dakta Huvisa wapewa meno kuanza zoezi la Bomoa Bomoa Nyumba zilizojengwa maeneo ya ufukweni


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL amekutana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa ANNA TIBAIJUKA na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Bi TEREZYA HUVISA, kwa mazungumzo na kupokea taarifa ya zoezi la bomoa bomoa ya nyumba zilizojengwa maeneo ua Ufukweni, ambalo linatarajia kuanza hivi karibuni,Mazungumzo hayo yamefanyika Ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu Dar es Salaam.

Katika picha kutoka (kushoto) ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka (kulia) ni Mkurugenzi wa Mazingira, Dkt, Julius Ningu na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt, Terezya Huvisa.

No comments:

Post a Comment