Wednesday, November 30, 2011

* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Bilal afunga mkutano wa nchi za maziwa makuu mjini Bujumbura


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Burundi Dkt JAMES MWASI baada ya kuwasili kwenye ukumbi wa Golf kwa ajili ya kufunga Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu, uliokuwa ukijadili Uendelezwaji wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED BILAL akisoma hotuba yake ya kufunga Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu.


Waziri wa Afrika Mashariki, SAMUEL SITTA akiwa katika Ukumbi wa Golf akimsikiliza kwa makini Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED BILAL alipokuwa akifunga rasmi Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu uliokuwa ukijadili Uendelezwaji wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika uliomalizika mjini Bujumbura nchini Burundi.

No comments:

Post a Comment