Sunday, November 13, 2011

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Shein atembelea kampuni ya Vifaa vya Ujenzi Huko Ras Al Khaimah


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt ALI MOHAMMED SHEIN, akizungumza na Sheikh SAUD Bin SAQR Al QASIMI ambae ni Mwenyeji wake na Kiongozi wa Ras Al Khaimah,wakati alipowasili katika kasri ya kiongozi huyo akiwa katika ziara ya kukuza uhusiano wa Ki-maendeleo katika sekta mbali mbali.


Rais wa Zanzibar  Dkt ALI SHEIN akikaribishwa na Naibu Mtendaji Mkuu wa kampuni ya ujenzi ya Rak Ceramics, Bwana ABDALLAH MASSAAD,wakati alipotembelea kuona vifaa mbali mbali vya ujenzi huko Ras Al Khaimah,akiwa katika ziara ya kukuza uhusiano na mashirikiano katika sekta za maendeleo.


Rais wa Zanzibar Dkt ALI  SHEIN akitembelea pamoja na kupata maelezo kutoka kwa Naibu Mtendaji Mkuu wa kampuni ya ujenzi ya Rak Ceramics ABDALLAH MASSAAD huko Ras Al Khaimah.

No comments:

Post a Comment