Monday, November 28, 2011

* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Bilal afungua Mkutano wa Viongozi wa Takukuru Mkoani Tanga


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Viongozi wa Takukuru Mkoani Tanga Kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Takukuru, EDWARD HOSEA kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga CHIKU GALAWA na waziri wa Ofisi ya Rais-Utawala Bora, MATHIAS CHIKAWE.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED BILAL akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Takukuru, EDWARD HOSEA mara baada ya kufungua rasmi mkutano Mkuu wa Viongozi wa Takukuru.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED BILAL akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Takukuru, EDWARD HOSEA wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Viongozi wa Takukuru, uliofanyika Mkoani Tanga Kushoto ni waziri wa Ofisi ya Rais- Utawala Bora, MATHIAS CHIKAWE.


Baadhi ya Wakuu wa Vitengo wa Takukuru waliohudhuria Mkutano huo Mkuu wa Mwaka ulioanza leo Novemba 28 na kumalizika kesho, Mkoani Tanga.

No comments:

Post a Comment