Friday, December 30, 2011

* Mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC John Ngahyoma afariki Dunia Jijini Dar es Salaam

Marehemu JOHN NGAHYOMA enzi ya Uhai wake

Mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC ya Uingereza, JOHN NGAHYOMA amefariki dunia leo asubuhi nyumbani kwake eneo la Segerea Jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Familia ya NGAHYOMA imesema kwamba Marehemu JOHN alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya Kansa katika ini iliyokuwa ikimsumbua kwa muda mrefu, ambapo amewahi kwenda kutibiwa mara mbili nchini INDIA.

Marehemu NGAHYOMA anatazamiwa kuzikwa siku ya Jumapili katika makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment