Friday, February 17, 2012

* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Bilal aendelea na Ziara yake Mkoani Ruvuma


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya uchimbaji Makaa ya Mawe ya Tancoal, GRAEME ROBERTSON, wakati alipotembelea mradi wa Uchimbaji Makaa ya Mawe unaoendelea eneo la Ruanda Wilaya ya Mbinga, wakati akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Ruvuma.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akiweka Jiwe la Msingi katika mradi wa mashine za kuzalisha umeme Wilayani Mbinga, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Ruvuma.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akibonyeza kitufe ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi mashine za kuzalisha umeme,Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Tanesco, Injinia BONIFACE NJOMBE.

No comments:

Post a Comment