Sunday, February 19, 2012

* Makamu wa Rais Dakta Mohammed Bilal akutana na mtafiti wa Masokwe hapa nchini


Makamu wa Rais  Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akipokea zawadi ya kitabu cha mtafiti bingwa duniani wa Masokwe, JANE GOODALL aliyefika Ikulu ndogo ya Wlaya ya Mpanda mkoa wa Katavi kwa ajili ya mazungumzo.

JANE amekaa nchini kwa miaka 50 akifanya utafiti katika mapori ya Gombe na Mahale yaliyopo mkoa wa Kigoma na Katavi.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL na mkewe Mama ASHA BILAL wakizungumza na Mtafiti bingwa wa Masokwe Duniani JANE GOODALL.



Makamu wa Rais Dkt MOHAMMED GHARIB BILAL akielekezwa na mtafiti bingwa Duniani wa Masokwe, JANE GOODALL kuhusu ishara anazozitumia kuwasiliana na Masokwe na jinsi ya kuzungumza nao, wakati alipofika Ikulu ndogo ya Wilaya ya Mpanda mkoa wa Katavi.

No comments:

Post a Comment