Saturday, July 2, 2011

* Makamu wa Rais Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL azindua rasmi Maonesho ya 35 ya Biashara ya Kimataifa Jijini Dar es Salaam


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL, akizindua rasmi maonyesho ya 35 ya Biashara  ya Kimataifa , wakati alipotembeleea maonyesho hayo katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere Barabara ya Kilwa Dar es Salaam.

 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL akimkabidhi Tuzo ya ushindi wa kundi la Engineering Products Mkurugenzi Mkuu wa Sido, MIKE LAISER,wakati wa ufunguzi rasmi wa maonyesho ya 35 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.


Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye pia ni Mkurugenzi wa Bendi ya Mjomba MRISHO MPOTO akitoa burudani mbele ya mgeni rasmi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta MOHAMMED GHARIB BILAL wakati wa uzinduzi wa maonyesho ya 35 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment