Thursday, September 15, 2011

Rais wa Visiwa vya Comoro Dakta IKILILOU DHOININE awasili nchini


Rais wa Visiwa vya Comoro Dakta IKHILILOU DHOININE amewasili nchini leo mchana akiwa ameambatana na ujumbe wake na kupokewa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta JAKAYA KIKWETE.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na maofisa wa Comoro zimeeleza kwamba lengo la ziara ya Dakta DHOININE ni kutoa pole kwa rais KIKWETE kutokana na vifo vya wananchi vilivyotokana na ajali ya meli ya Mv SPICE ISLANDER iliyokuwa ikitokea Unguja kuelekea Pemba.

No comments:

Post a Comment