Monday, September 19, 2011

* Rais wa Zanzibar Dakta Ali Mohammed Shein akutana na wananchi wa Visiwa vya Pemba na kuwapa Pole kutoka na Msiba wa ajali ya Mv Spice Islander's


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dakt  ALI MOHAMMED SHEIN akitia saini kitabu cha wageni alipowasili katika skuli ya Piki, kuzungumza na wananchi wa familia 70 wa Kisiwani Piki na Mzambaun Takao, waliofiliwa na jamaa zao katika ajali ya Meli ya Mv SPICE ISLANDER'S ,hivi karibuni,akiwa katika ziara maalum ya kuwapa pole wananchi waliopatwa na Msiba wa jamaa zao katika kisiwa cha Pemba.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dakta ALI MOHAMMED SHEIN akizungumza na akizungumza na wananchi wa Daya Mtambwe wakati alipofika kuwapa Pole na kuwahutubia.




Baadhi ya wananchi wa familia zaidi ya 70 wa Kisiwa cha Piki na Mzambarun takao, wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dakta ALI MOHAMMED SHEIN, alipofika Skuli ya Sekondari ya Piki kuwapa pole kutokana na ajali ya kuzama kwa Meli ya Mv SPICE ISLANDER'S hivi karibuni .

No comments:

Post a Comment